Msigwa: Serikali itafanyia kazi haraka maazimio ya kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imesema itahakikisha inafanyia kazi mapendekezo yote yatakayotolewa kwenye maazimio ya pamoja ya Waandishi wa Habari baada ya kuhitimisha Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari kwa mwaka 2025.

Hakikisho hilo la Serikali limetolewa Aprili 28, 2025 na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson wakati akitoa neno la kufunga Siku ya Kwanza ya Kongamano hilo linalofanyika jijini Arusha kwa uratibu wa Jamii Africa, UNESCO na Wizara yenyewe.

“Nimesikia maazimio ya awali mliyoyatoa hapa, ni muhimu sana na mimi nitaomba mkishakamilisha ile nakala ya mwisho mtupatie ili na sisi serikalini yale ambayo tunatakiwa tuchukue hatua tuyafanyie kazi, basi tutafanyia kazi mara moja”, amesema Msigwa.

Amewapongeza wadau wote walioshiriki Kongamano hilo na kwa majadiliano waliyoyafanya ikiwemo suala la matumizi ya Akili Mnemba kwa kuwa ni jambo muhimu kwenye kazi za uandishi wa habari kwa sasa.

Msigwa amesema Serikali itaendelea kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari nchini na kwamba hilo linajidhihirisha kwani kumekuwa na mazingira rafiki kwa Waandishi wa Habari pale wanapotekeleza majukumu yao.

“Sisi Waandishi wa Habari kwenye Awamu hii ya sita tumekuwa tukifanya kazi katika mazingira rafiki sana, kwa sababu ya maelekezo ambayo Mheshimiwa Rais (Samia Suluhu Hassan) anayasimamia,” amesisitiza Msigwa na kuongeza:

“Aliyoyasema tangu siku ya kwanza alipoingia madarakani ndiyo anayoyatekeleza na sisi lazima tutekeleze maelekezo yake kuhakikisha kuna uhuru wa vyombo vya habari, kuhakikisha waandishi wa Habari hawabughudhiwi lakini kuendelea kujenga mazingira bora kwa waandishi wa habari kufanya kazi zao,”.

Kongamano hilo la Maadhimisho ya Siku ya Siku ya Uhuru wa Habari linatarajiwa kufungwa leo Aprili 29, 2025 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...