Mkoa wa Mwanza wawakaribisha wawekezaji, waanika fursa lukuki

Na Winfrida Mtoi, Mwanza

MKOA wa Mwanza umeweka bayana utayari wake wa kutoa maeneo ya uwekezaji kwa watu binafsi na Serikali kutokana na fursa nyingi zinazopatikana katika mkoa huo.

Hayo yameelezwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Chagu Nghoma alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa huo, Said Mtanda katika Mdahalo wa Kitaifa uliondaliwa na Kituo cha Ubia wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) wenye Mada Kuu ya ‘Ubia wa Sekta ya umma na Sekta Binafsi katika Muktadha wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 uliofanyika kwenye Ukumbi wa hoteli ya Gold Crest, jijini Mwanza.

Mhandisi Nghoma amesema kuna fursa nyingi ya uwekezaji za kukuza uchumi katika Mkoa huo, ikiwamo sekta ya Uchumi wa Buluu ukilenga ufugaji wa samaki na shughuli nyingine zinazofanyika katika Ziwa Victoria.

Amesema pamoja na hayo pia kuna maeneo mengi yanayofaa kwa ufugaji wa mifungo kama vile Ng’ombe na Mbuzi.

Ameeleza kuwa kuhusu uchumi wa Buluu kuna ufugaji wa samaki ambayo inahitaji kwa kiasi kikubwa uwekezaji wa viwanda na kuwekeza katika chakula cha samaki, pia viwanda vya nyama vinahitajika zaidi.

“Mkoa wa Mwanza una maeneo mengi ya uwekezaji na Mkoa upo tayari kuyatoa maeneo hayo kwa watu binafsi na Serikali. Uchumi wa mtu unaanza na mtu binafsi, ni lazima kufikiria nini unataka kufanya katika kuboresha uchumi binafsi na nchi,” amesema.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...