YANGA YAIBAMIZA AZAM, TABORA HALI TETE, COASTAL YAZINDUKIA MKWAKWANI

Na Mwandishi Wetu

Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Yanga yalifungwa na Pacome Zouzoua dk 11, Prince Dube dk 34 wakati la Azam likifungwa na Lusajo Mwaikenda dk 81.

Wakati huo huo timu ya Tabora United imepoteza mchezo wa nne mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya leo Aprili 10, 2025 kufungwa mabao 3-0 na Mashujaa FC katika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.

Kabla ya mchezo wa leo ilitoka kufungwa na Pamba 1-0, CCM Kirumba, Mwanza, imepoteza nyumbani dhidi ya Yanga 3-0, na JKT Tanzania iliifunga 2-1.

Nayo Coastal Union baada ya kukosa ushindi katika michezo nane mfululizo leo imezinduka kwa kuifunga Singida BS mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga.

spot_img

Latest articles

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

More like this

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...