PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia utekelezaji wa agenda ya Nishati Safi ya kupikia iliyoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa imeanza kutekelezwa kwa vitendo na kuonyesha mafanikio makubwa.

Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba, Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Charles Sangweni, amesema mwitikio wa wananchi kuhusu nishati safi umekuwa mkubwa, na kwamba mamlaka hiyo imejipanga kuhakikisha haina mwanya wa kumuangusha Rais katika agenda hiyo muhimu ya kitaifa.

“Katika maonesho haya ya Sabasaba, tumeona mwamko mkubwa wa wananchi katika masuala ya nishati safi ya kupikia. Hii inaonyesha uelewa unaongezeka, na sisi kama PURA tunaitekeleza agenda hii kikamilifu,” amesema Sangweni.

Ameeleza kuwa PURA imekuwa mshiriki wa kudumu wa maonesho hayo tangu mwaka 2017, na kwamba kila mwaka kumekuwa na maboresho ya kimkakati katika ushiriki wao.

Kwa mwaka huu, amesema, mambo yameimarika zaidi, hasa kwenye matumizi ya mifumo ya kidijitali na ongezeko la idadi ya wananchi wanaotembelea banda lao.

“Watu wanauliza maswali ya msingi, yenye maana na yanayoonyesha namna uelewa kuhusu sekta ya mafuta na gesi ulivyopanuka. Tunapokea maoni, changamoto na maulizo ambayo yanatusaidia pia kuboresha utendaji wetu,” amesema.

Akizungumzia nafasi ya Watanzania katika sekta ya mafuta na gesi, Sangweni amesema tangu kuanzishwa kwa PURA, kumekuwa na ongezeko kubwa la ushiriki wa Watanzania, ambapo kwa sasa asilimia 85 ya ajira katika sekta hiyo zinashikiliwa na wazawa, ikilinganishwa na chini ya asilimia 55 hapo awali.

“Uzoefu na uelewa vimeongezeka. Awali meli zilikuja na wafanyakazi kutoka nje pekee, lakini sasa hata Watanzania wapo ndani ya timu hizo. Hili ni jambo la kujivunia,” amesema.

Kwa mujibu wa Sangweni, PURA kwa sasa iko kwenye maandalizi ya kuchimba visima vitatu katika eneo la Mtwara, huku ushiriki wa Watanzania katika vitalu hivyo ukiwa umefikia asilimia 40.

Pia amesema kati ya kampuni 10 zinazofanya utafiti wa mafuta na gesi nchini, sita zinamilikiwa na Watanzania.

“Kwenye nafasi za uongozi ndani ya sekta, karibu asilimia 95 zinashikiliwa na Watanzania. Hii inadhihirisha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha rasilimali zetu zinawanufaisha wananchi,” amesema.

Ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji na ushirikishwaji wa Watanzania katika miradi ya kimkakati, akisisitiza kuwa PURA itaendelea kuhakikisha kila hatua ya maendeleo inawagusa Watanzania moja kwa moja.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...