Mgodi mkubwa wa dhahabu kuanzishwa Hanang’-Manyara

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Aprili 9, 2025 amefanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Marvel Gold, Timothy Strong juu ya uwekezaji wa kampuni hiyo kwenye sekta ya madini.

Kampuni hiyo kutoka nchini Australia imefika kujitambulisha na kuelezea mpango wao wa kuanzisha mgodi mkubwa wa dhahabu katika Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara.

“Tumeichagua Tanzania kwasababu ni nchi ambayo ina amani na usalama na mazingira mazuri ya uwekezaji,na tumevutiwa na mpango mzuri wa Rais Dkt. Samia S. Hassan kuvutia uwekezaji nchini Tanzania,” amesema Strong.

Ameongeza kwamba, kampuni hiyo itafanya utafiti wa kina kwa kurusha ndege na baadaye kukamilisha hatua zote za utafiti wa madini.

Ameeleza kuwa, kampuni hiyo inategemea kuanza zoezi la utafiti wa kina ifikapo mwezi Septemba 2025.

Awali, akizungumza katika kikao hicho, Waziri Mavunde amewapongeza wadau hao kwa kuichagua Tanzania kufanya uwekezaji wao na kuwahakikishia kwamba serikali itatoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha miradi kama hiyo yenye dhamira ya kukuza sekta ya madini inafanikiwa.

“Ninapokea watu wengi sana wenye nia kama ya kwenu, asilimia kubwa si wakweli kutekeleza mipango yao na wamekuwa na maneno mengi kuliko vitendo,” amesema Waziri Mavunde.

Ameongeza kwamba ana amini kwamba Kampuni hiyo itafanya kazi kubwa ya utafiti ili kama nchi ifanikiwe kupata mradi mwingine mkubwa wa uchimbaji madini ya dhahabu Mkoani Manyara.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...