Kapinga: Vitongoji 9000 kusambaziwa umeme mwaka 2025/26

📌 Majimbo yaendelea kufaidika na mradi wa umeme wa Vitongoji 15

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha kazi ya kupeleka umeme kwenye Vijiji vyote Tanzania Bara na nguvu sasa inaelekezwa kwenye vitongoji.

Kapinga ameeleza kuwa, pamoja na kazi ya kupeleka umeme vitongojini inayoendelea sasa, Serikali ina mkakati wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji 9,000 katika mwaka ujao wa fedha wa 2025/26.

Ameeleza hayo leo Aprili 09, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Nkansi Kusini, Vicent Mbogo aliyeuliza ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji vilivyopo Jimbo la Nkansi Kusini.

“Kitongoji cha Lupata kilichopo Kata ya Kizumbi kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya kila Mbunge, na kitongoji cha Lwela Kata ya Mpembe kitapata umeme kupitia miradi itakayokuja,” amesema Kapinga.

Akijibu swali Mbunge wa Momba, Condester Sichwale aliyeuliza ni upi mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji vya Tarafa za Ndarambu, Msangano na Kamsambu, Kapinga amesema Serikali inao mkakati wa kutekeleza miradi ya umeme kwenye Vitongoji na hivi sasa inatekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji 15 kwa kila Jimbo.

Ameongeza kuwa katika miradi wa Vitongoji 15 wakandarasi wamemaliza kazi za awali na sasa hivi wapo katika hatua ya kupata vifaa.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...