Tanesco yashinda tena Tuzo za Ubora Huduma kwa Wateja za CICM

📌Urahisi wa upatikanaji whuduma kwa njia za kidigitali watajwa moja ya kigezo cha kushinda tuzo hiyo

📌MD Gissima aibuka kidedea kwa Kusimamia Maboresho yenye tija huduma kwa wateja Sekta ya Umma.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la umeme Tanzania (TANESCO) kwa mara nyingine tena limeshinda tuzo ya the ”Most improved Organization” eneo la huduma kwa wateja iliyotolewa na Taasisi ya Chartered Institute of Customer Management(CICM).

Tuzo hizo zimetolewa 28, Machi 2025 jijini Dar es Salaam ambapo Shirika limepata tuzo hiyo baada ya kufanya maboresho ya kutumia njia za kidigitali kurahisisha mchakato wa maombi ya umeme na upatikanaji wa huduma kuwa mwepesi kwa wateja wake.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO , Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Irene Gowelle amesema Tuzo hizo ni heshima kwa Shirika ikiwa ni ishara nzuri ya maboresho yanayofanyika kutambuliwa na kuthaminiwa.

“Tuzo hizi ni heshima kubwa kwa TANESCO, zinatuongezea ari ya kufanya vizuri zaidi,tutaongeza ubunifu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja wetu,’’.

Aidha , Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mha. Gissima Nyamo-Hanga na yeye alishinda Tuzo ya heshima ya Kiongozi anayefanya mabadiliko chanya yenye tija upande wa huduma kwa wateja katika Sekta ya Umma.

Tuzo za Tanzania Service excellence awards hutolewa kila mwaka na zinalenga kutambua Taasisi za Umma na binafsi zinazoimarisha na kuboresha huduma bora kwa wateja wake.

spot_img

Latest articles

FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa...

Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara...

Kada wa Chadema amuomba msajili wa vyama vya siasa kubatilisha Baraza Kuu la chama hicho lililoketi Januari 22, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Mwanga,...

GSM, EFTA zaungana kuwabeba wafanyabiashara wadogo na kati

Na Mwandishi Wetu Taasisi ya kifedha ya EFTA na GSM zimeungana kwa kusaini mkataba wa...

More like this

FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa...

Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara...

Kada wa Chadema amuomba msajili wa vyama vya siasa kubatilisha Baraza Kuu la chama hicho lililoketi Januari 22, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Mwanga,...