GF Automobile, NaCoNGO zasaini makubaliano ya kimkakati kusaidia vijana

Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya GF Trucks kupitia kampuni ya GF Automobile imeingia makubaliano na Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini (NaCoNGO ), yakilenga kunufaisha pande zote mbili katika nyanja mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya GF Trucks ,Mujtaba Karmali amesema wao kama wauzaji wa magari na mitambo wameoana kuna haja ya kuingia makubaliano hayo ya kimkakati ambapo pia watatoa elimu, kuwajengea uwezo na uelewa katika maeneo tofauti.

Aidha Karmali amesema tayari wao wameanza mpango wa kutoa mafunzo kazi kwa vijana wanaomaliza vyuo mbalimbali mfano , VETA na DIT ili kuwajengea uwezo wa kuweza kufanya kazi na kupata uzoefu kazini.

” Makubaliano haya yatarahisisha kuwafikia makundi ya vijana nchi nzima na kuungana na serikali katika mpango wa kuhakikisha vijana wanajengewa uwezo wa kuajiriwa na kujiajiri kwa kupita katika vyuo mbalimbali,” ameeleza Karmali.

Nae Mwenyekiti wa NaCoNGO , Jasper Makala ameishukuru kampuni ya GF Trucks kwa kuonyesha njia kwa makampuni ya Kitanzania kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali.

Amesisitiza kuwa ushirikiano na makampuni binafsi ya ndani ya nchi ni mbinu mojawapo ya kupunguza utegemezi toka nje ya nchi kuelekea katika uendelevu wa mashirika.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...