GF Automobile, NaCoNGO zasaini makubaliano ya kimkakati kusaidia vijana

Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya GF Trucks kupitia kampuni ya GF Automobile imeingia makubaliano na Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini (NaCoNGO ), yakilenga kunufaisha pande zote mbili katika nyanja mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya GF Trucks ,Mujtaba Karmali amesema wao kama wauzaji wa magari na mitambo wameoana kuna haja ya kuingia makubaliano hayo ya kimkakati ambapo pia watatoa elimu, kuwajengea uwezo na uelewa katika maeneo tofauti.

Aidha Karmali amesema tayari wao wameanza mpango wa kutoa mafunzo kazi kwa vijana wanaomaliza vyuo mbalimbali mfano , VETA na DIT ili kuwajengea uwezo wa kuweza kufanya kazi na kupata uzoefu kazini.

” Makubaliano haya yatarahisisha kuwafikia makundi ya vijana nchi nzima na kuungana na serikali katika mpango wa kuhakikisha vijana wanajengewa uwezo wa kuajiriwa na kujiajiri kwa kupita katika vyuo mbalimbali,” ameeleza Karmali.

Nae Mwenyekiti wa NaCoNGO , Jasper Makala ameishukuru kampuni ya GF Trucks kwa kuonyesha njia kwa makampuni ya Kitanzania kuchangia maendeleo ya jamii kupitia mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali.

Amesisitiza kuwa ushirikiano na makampuni binafsi ya ndani ya nchi ni mbinu mojawapo ya kupunguza utegemezi toka nje ya nchi kuelekea katika uendelevu wa mashirika.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...