VETA yafadhili mafunzo kwa wanawake 3000 jijini Dodoma

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetoa ufadhili wa mafunzo ya muda mfupi kwa wanawake 3000 jijiji Dodoma, yatakayotolewa katika Chuo cha VETA Dodoma.

Akizungumza jana, tarehe 24 Machi, 2025 wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo hayo yanayotolewa kupitia kikundi cha Wanawake na Samia, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amemshukuru Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Anthony Kasore kwa ufadhili wa mfunzo hayo.

Senyamule amesema wanawake wengi, hawana ujuzi, hivyo mafunzo ya stadi kwao ni muhimu ili kuwawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

“Dodoma sasa ni mji wa kitalii na watu wengi wanakuja kwa ajili ya kupata huduma sa Kiserikali. Wapo wengine kutoka mataifa mbalimbali. Hivyo tunahitajika kutoa huduma za kiwango cha kimataifa na hilo linawezekana ikiwa tutapata mafunzo,” amesema Senyamule.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma, Fatuma Madidi ametoa pongezi kwa Mkurugenzi Mkuu wa VETA na Mkuu wa chuo cha VETA Dodoma kwa kuridhia mafunzo hayo kutolewa kwa wanwake wa Dodoma kupitia chuo cha VETA Dodoma.

“Ukimsomesha mwanamke umesomesha jamii nzima, tunaahidi kuwa watulivi na kujifunza kwa bidii,” amesema Madidi.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Kasore amesema VETA itagharamia mafunzo hayo kwa wanawake na Samia na kuongeza kuwa anaamini ujuzi watakaoupata utawasaidia kuendesha shughuli zao za uzalishaji na kujingiizia kipato.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...