Ewura yaendelea kuweka mazingira rafiki kwa uwekezaji wa CNG nchini

Na Mwandishi Wetu 

Mkurugenzi wa Gesi Asilia wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mha. Poline Msuya, amesema EWURA inaendelea kuweka mazingira rafiki ya kuhamasisha uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa biashara ya gesi asilia iliyogandamizwa (CNG) ikiwa ni hatua muhimu katika kusaidia juhudi za Serikali za kuchochea matumizi ya nishati safi nchini.

Msuya ameyasema hayo wakati wa majadiliano ya jopo katika mkutano wa awali wa Mkutano wa 11 wa Mafuta na Gesi wa Afrika Mashariki (EAPCE’25) uliofanyika leo tarehe 04.03.2025 jijini Dar es Salaam. Mkutano husika ambao ni wa siku tatu utaanza rasmi kesho tarehe 05.03.2025.

Ameeleza kuwa moja ya hatua muhimu zilizokwisha kuchukuliwa kuhamasisha uwekezaji ni pamoja na kuondolewa kwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye miundombinu muhimu ya CNG, ikiwa ni pamoja na mashine za kushindilia gesi (compressors), vitengo vya kupima gesi (metering units), na hifadhi za CNG (storage cascades) jambo linalovutia uwekezaji zaidi katika sekta husika.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...