Ewura yaendelea kuweka mazingira rafiki kwa uwekezaji wa CNG nchini

Na Mwandishi Wetu 

Mkurugenzi wa Gesi Asilia wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mha. Poline Msuya, amesema EWURA inaendelea kuweka mazingira rafiki ya kuhamasisha uwekezaji katika mnyororo wa thamani wa biashara ya gesi asilia iliyogandamizwa (CNG) ikiwa ni hatua muhimu katika kusaidia juhudi za Serikali za kuchochea matumizi ya nishati safi nchini.

Msuya ameyasema hayo wakati wa majadiliano ya jopo katika mkutano wa awali wa Mkutano wa 11 wa Mafuta na Gesi wa Afrika Mashariki (EAPCE’25) uliofanyika leo tarehe 04.03.2025 jijini Dar es Salaam. Mkutano husika ambao ni wa siku tatu utaanza rasmi kesho tarehe 05.03.2025.

Ameeleza kuwa moja ya hatua muhimu zilizokwisha kuchukuliwa kuhamasisha uwekezaji ni pamoja na kuondolewa kwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye miundombinu muhimu ya CNG, ikiwa ni pamoja na mashine za kushindilia gesi (compressors), vitengo vya kupima gesi (metering units), na hifadhi za CNG (storage cascades) jambo linalovutia uwekezaji zaidi katika sekta husika.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

More like this

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...