Wasira: Vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika viendeshwe kwa kuzingatia mahitaji

Na Mwandishi Wetu

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema vyama ya ukombozi kusini mwa Afrika viendeshwe Kwa kuzingatia mahitaji ya wakati huu bila kusahau shabaha ya kuanzishwa kwake.

Amesema kuwa vyama hivyo vilipigania uhuru kuzikomboa jamii za waafrika ambayo ndani yake ina vizazi vilivyopo na vinavyokuja.Wasira ameeleza hayo leo Machi 3, 2024 alipokuwa akifungua semina kwa viongozi vijana kutoka vyama vya ukombozi Kusini mwa Afrika iliyofanyika katika Shule ya Uongozi ya Julius Kambarage Nyerere, Kibaha mkoani Pwani.

Vyama hivyo ni FRELIMO (Msumbuji), MPLA (Angola), ANC (Afrika Kusini), SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe) na CCM (Tanzania) ambapo katika mapambano ya ukombozi vilishirikiana kwa karibu na Chama cha Kikomist cha China (CPC).

Amesema lengo la semina hiyo ni kuimarisha vyama hivyo ambapo anaamini mifumo ya siasa inabadilika kutoka chama kimoja kwenda vyama vingi na lazima kutafuta mbinu ambayo itavifanya vyama hivyo kujiimarisha kutoka chini, visiwe vyama vya watu wachache hatua ambayo inalenga kuhakikisha vinaendelea kuongoza nchi zao.

“Mbinu za kuongoza nchi zao ni kuhakikisha mabadiliko yoyote ya dunia hayayumbishwi lakini pamoja na kwamba ni lazima washirikiane na dunia nyingine wasifanye dunia ikawa badala ya shabaha yao, maana duniani hapa kuna mambo yake vilevile.

“Vyama hivi shabaha yake ni ya muda mrefu ambayo ni kuona dunia ina maisha bora kwa watu wake ambao wanazaliwa kila siku, hata kama kuna mabadiliko mengi yanatokea shabaha inabaki ile ile kuona watu wetu katika nchi hizi wanapata maisha mazuri na hii ndio shabaha ya msingi na haina mwisho, huwezi kusema maisha sasa yametosha,” amesema.

Akizungumzia nafasi ya vijana, amesema ndio warithi halali wa vyama hivyo, hata yeye alikuwa kijana na hiyo inamaanisha kuwa hakuna kuendelea bila kijana.Kwa mujibu wa Wasira, urithi wa vijana ni muhimu kwa maendeleo ya vyama hivyo na kwamba kama haikufanyika hivyo vitakuwa vyama vya wazee ambao wakiondoka na vyama vinaondoka.

“Ni lazima kurithisha vijana ili wachukue nafasi yao katika kuongoza vyama hivyo. Sio kila kijana anaweza kurithi, wanatakiwa vijana wanaojua historia, wanaojua sababu ya hivi vyama kwa nini wazee wao walipigana hadi wakafa, wakijua hivyo wataendeleza shabaha iliyowaua wale.

“Tumeanza tunachukua chipukizi na UVCCM kuwapeleka Ihemi, Iringa kuwafundisha, hapa katikati tulikuwa tumeacha hiyo program lakini sasa tumejua bila mafunzo tutapata tabu kurithisha uongozi unaoeleweka, tunawafundisha itikadi ya vyama hivi na shabaha yake,” amesema.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...