Zaidi ya watu 50 wafariki Congo kwa ugonjwa usiojulikana

Na Mwandishi Wetu 

ZAIDI ya watu 50 wamefariki Kaskazini Magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na ugonjwa usiojulikana.

Mkurugenzi wa hospitali ya Bikoro, kituo cha ufuatiliaji wa afya, Serge Ngalebato, ameliambia shirika la habari la AP kwamba muda kati ya kuanza kwa dalili na kifo ni saa 48 kwa wagonjwa wengi.

Ngalebato amesema hali hiyo inatia wasiwasi na mlipuko wa ugonjwa huo usiojulikana ulitokea mnamo Januari 21 na hadi sasa wagonjwa 419 wameripotiwa, ikiwemo vifo vya watu 53.

Kwa mujibu wa ofisi ya WHO barani Afrika, mlipuko wa kwanza katika mji wa Boloko ulitokea baada ya watoto watatu kula popo na kufariki ndani ya saa 48 baada ya kuonyesha dalili za homa na kutokwa na damu.

Mwaka jana, ugonjwa mwengine usiojulikana ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 100 kusini magharibi mwa Kongo japo baadaye iligundulika kuwa ni aina kali ya malaria.

Source: DW

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

More like this

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...