Zaidi ya watu 50 wafariki Congo kwa ugonjwa usiojulikana

Na Mwandishi Wetu 

ZAIDI ya watu 50 wamefariki Kaskazini Magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na ugonjwa usiojulikana.

Mkurugenzi wa hospitali ya Bikoro, kituo cha ufuatiliaji wa afya, Serge Ngalebato, ameliambia shirika la habari la AP kwamba muda kati ya kuanza kwa dalili na kifo ni saa 48 kwa wagonjwa wengi.

Ngalebato amesema hali hiyo inatia wasiwasi na mlipuko wa ugonjwa huo usiojulikana ulitokea mnamo Januari 21 na hadi sasa wagonjwa 419 wameripotiwa, ikiwemo vifo vya watu 53.

Kwa mujibu wa ofisi ya WHO barani Afrika, mlipuko wa kwanza katika mji wa Boloko ulitokea baada ya watoto watatu kula popo na kufariki ndani ya saa 48 baada ya kuonyesha dalili za homa na kutokwa na damu.

Mwaka jana, ugonjwa mwengine usiojulikana ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 100 kusini magharibi mwa Kongo japo baadaye iligundulika kuwa ni aina kali ya malaria.

Source: DW

spot_img

Latest articles

GST: Taarifa sahihi za kijiolojia ni msingi wa uchimbaji wenye tija

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imewataka wachimbaji,...

NIC: Waandishi wa habari vinara wa kuhamasisha matumizi ya bima

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC Insurance) limewapongeza waandishi wa habari...

TAIC: Bima ya kilimo ni kinga ya mtaji wa wakulima na wafugaji

Na Mwandishi Wetu UMOJA wa Makampuni ya Bima za Kilimo Tanzania (TAIC) umewahimiza wakulima...

TIRA yatumia Nanenane kuhamasisha wakulima kujiunga na bima ya kilimo

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imetumia Maonesho ya Kimataifa ya...

More like this

GST: Taarifa sahihi za kijiolojia ni msingi wa uchimbaji wenye tija

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imewataka wachimbaji,...

NIC: Waandishi wa habari vinara wa kuhamasisha matumizi ya bima

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC Insurance) limewapongeza waandishi wa habari...

TAIC: Bima ya kilimo ni kinga ya mtaji wa wakulima na wafugaji

Na Mwandishi Wetu UMOJA wa Makampuni ya Bima za Kilimo Tanzania (TAIC) umewahimiza wakulima...