Zaidi ya watu 50 wafariki Congo kwa ugonjwa usiojulikana

Na Mwandishi Wetu 

ZAIDI ya watu 50 wamefariki Kaskazini Magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na ugonjwa usiojulikana.

Mkurugenzi wa hospitali ya Bikoro, kituo cha ufuatiliaji wa afya, Serge Ngalebato, ameliambia shirika la habari la AP kwamba muda kati ya kuanza kwa dalili na kifo ni saa 48 kwa wagonjwa wengi.

Ngalebato amesema hali hiyo inatia wasiwasi na mlipuko wa ugonjwa huo usiojulikana ulitokea mnamo Januari 21 na hadi sasa wagonjwa 419 wameripotiwa, ikiwemo vifo vya watu 53.

Kwa mujibu wa ofisi ya WHO barani Afrika, mlipuko wa kwanza katika mji wa Boloko ulitokea baada ya watoto watatu kula popo na kufariki ndani ya saa 48 baada ya kuonyesha dalili za homa na kutokwa na damu.

Mwaka jana, ugonjwa mwengine usiojulikana ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 100 kusini magharibi mwa Kongo japo baadaye iligundulika kuwa ni aina kali ya malaria.

Source: DW

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...