Zaidi ya watu 50 wafariki Congo kwa ugonjwa usiojulikana

Na Mwandishi Wetu 

ZAIDI ya watu 50 wamefariki Kaskazini Magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na ugonjwa usiojulikana.

Mkurugenzi wa hospitali ya Bikoro, kituo cha ufuatiliaji wa afya, Serge Ngalebato, ameliambia shirika la habari la AP kwamba muda kati ya kuanza kwa dalili na kifo ni saa 48 kwa wagonjwa wengi.

Ngalebato amesema hali hiyo inatia wasiwasi na mlipuko wa ugonjwa huo usiojulikana ulitokea mnamo Januari 21 na hadi sasa wagonjwa 419 wameripotiwa, ikiwemo vifo vya watu 53.

Kwa mujibu wa ofisi ya WHO barani Afrika, mlipuko wa kwanza katika mji wa Boloko ulitokea baada ya watoto watatu kula popo na kufariki ndani ya saa 48 baada ya kuonyesha dalili za homa na kutokwa na damu.

Mwaka jana, ugonjwa mwengine usiojulikana ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 100 kusini magharibi mwa Kongo japo baadaye iligundulika kuwa ni aina kali ya malaria.

Source: DW

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...