Ndejembi amsimamisha kazi Afisa ardhi Handeni

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Deogratius Ndejembi amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Anthony Sanga kumsimamisha kazi na kumchukulia hatua za kinidhamu, Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Mji Handeni kwa kuwa chanzo cha migogoro ya ardhi kwenye Halmashauri hiyo.

Ndejembi ametoa agizo hilo Januari 20, 2025 alipofanya ziara katika Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga ambapo alitembelea eneo la Kwanjugo Kitalu A ambalo wananchi wake wamekua wakilalamika kwa muda mrefu kuchukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia.

“Hapa kiasili pana historia yake, palikua pana umiliki wa wenyewe sasa haiwezekani watu hawa kuonewa, na migogoro yote hii ni kwa sababu hatusikilizi wananchi wetu, sasa ninamuelekeza Katibu Mkuu kumsimamisha mara moja Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Halmashauri na haraka sana aletwe mtu mwingine atakayeweza kutatua migogoro ya ardhi Handeni.

“Lakini pia ninaelekeza kuundwa kwa Timu ya uchunguzi itakayokua chini ya Kamishna wa Ardhi, ije hapa Handeni ndani ya wiki moja ili ichunguze umiliki wa viwanja vya sasa ni akina nani, na kama ni watumishi wa ardhi tuchukue hatua kali. Kwa sababu hatuwezi kuruhusu watumishi wa ardhi kunyang’anya ardhi ya wananchi,” amesema Ndejembi.

spot_img

Latest articles

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...