Mhandisi Bwire: Tunairudisha Dawasa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed, Dar es Salaam

KAIMU Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Mkama Bwire amesema wanakusudia kurejesha Mamlaka hiyo kwa wananchi ili kutoa fursa na na nafasi ya kufikisha mrejesho wa huduma na kutatua changamoto za Maji ili kusaidiwa kwa haraka.

Mhandisi Bwire ameyasema hayo leo Februari 20, 2025 wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi kati ya DAWASA na Wenyeviti wa mitaa wa wilaya ya Temeke na kusema kuwa hiyo ndio agenda ya Mamlaka katika utendaji kazi wao.

“Tunekusudia turudishe DAWASA iwe ni ya wananchi tunaamini tukishirikiana pamoja changamoto za kihuduna kupitia Wenyeviti wa mitaa zitaisha,” amesisitiza Mhandisi Bwire

Amesema kupitia kikao hicho watajadili changamoto za maji zilizopo katika maeneo ya Temeke kupokea mawazo na maoni ya wenyeviti juu ya suluhisho lakini kujenga mahusiano yatakayosaidia kuweza kuwa karibu baina ya DAWASA na viongozi hao.

“Lazima tuwe na mambo ambayo tunataka kushirikiana na kujenga uelewa wa pamoja tunapoenda kwa Wananchi kile anachozungumza Mwenyekiti na DAWASA azungumze hivyo,” amesisitiza

Aidha Mhandisi Bwire ameongeza kuwa mamlaka hiyo imetambua umuhimu wa wenyeviti na kuelewa nafasi yao katika kurahisisha ufikishaji wa huduma kwa Wananchi na kutatua changamoto zilizopo.

Pamoja na hayo Mhandisi Bwire amekiri uwepo wa changamoto mbalimbali katika Manispaa ya Temeke lakini amesema anaamini sasa itakuwa rahisi kutatua changamoto hizo kutokana na uwepo wa uhusiano mzuri baina yao.

Mwisho 

spot_img

Latest articles

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...