Watu watatu wafariki kwa ajali Kimara Stop Over

Na Mwandishi Wetu

WATU watatu wafariki na wengine wamejeruhiwa kwenye ajali iliyotokea usiku wa kuamkia Februari 14,2025 katika Mtaa wa Kimara Stop Over.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema ajali imehusisha lori lililohama njia na kuparamia kituo cha bodaboda kilichopo Kimara Stop Over.

Amesema Lori hilo lilikuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam na katika ajali hiyo hadi saa 9:00 alfajiri miili mitatu iliyokuwa imekandamizwa na kontena la lori hilo imeshatolewa.

“Miili ya watu hawa inasemekana walikuwa madereva pikipiki, pia tumefanikiwa kutoa pikipiki ambazo kwa idadi ni nyingi kuliko watu tuliowakuta kwa mantiki hiyo taarifa ya Polisi itaweka bayana,” amesema Chalamila.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi amesema kutokana na idadi ya pikipiki kuwa kubwa kuliko miili iliyokutwa, inawezekana wakati wa tukio watu walikimbia kujiokoa.

“Taarifa kwa kirefu tutaitoa tukishajua chanzo cha ajali hii kwa kuwa imetokea usiku na tumekuwa hapa kwa zaidi ya saa mbili,” amesema Kamanda Kitinkwi.

Baadhi ya mashuhuda wanasema gari hilo lilifeli brake na kukwepa daladala zilizokuwa zimebaki kwenye zebra na kuangukia watu waliokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara pamoja na pikipiki 15, zilizokuwa zimeegeshwa kwenye eneo hilo.

spot_img

Latest articles

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

More like this

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...