Watu watatu wafariki kwa ajali Kimara Stop Over

Na Mwandishi Wetu

WATU watatu wafariki na wengine wamejeruhiwa kwenye ajali iliyotokea usiku wa kuamkia Februari 14,2025 katika Mtaa wa Kimara Stop Over.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema ajali imehusisha lori lililohama njia na kuparamia kituo cha bodaboda kilichopo Kimara Stop Over.

Amesema Lori hilo lilikuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam na katika ajali hiyo hadi saa 9:00 alfajiri miili mitatu iliyokuwa imekandamizwa na kontena la lori hilo imeshatolewa.

“Miili ya watu hawa inasemekana walikuwa madereva pikipiki, pia tumefanikiwa kutoa pikipiki ambazo kwa idadi ni nyingi kuliko watu tuliowakuta kwa mantiki hiyo taarifa ya Polisi itaweka bayana,” amesema Chalamila.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi amesema kutokana na idadi ya pikipiki kuwa kubwa kuliko miili iliyokutwa, inawezekana wakati wa tukio watu walikimbia kujiokoa.

“Taarifa kwa kirefu tutaitoa tukishajua chanzo cha ajali hii kwa kuwa imetokea usiku na tumekuwa hapa kwa zaidi ya saa mbili,” amesema Kamanda Kitinkwi.

Baadhi ya mashuhuda wanasema gari hilo lilifeli brake na kukwepa daladala zilizokuwa zimebaki kwenye zebra na kuangukia watu waliokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara pamoja na pikipiki 15, zilizokuwa zimeegeshwa kwenye eneo hilo.

spot_img

Latest articles

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

Dkt. Mwigulu aweka jiwe la Msingi Mradi wa Umeme Mkata

Ni ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 60 📌Mradi...

Ithibati yatajwa kuimarisha uaminifu wa Sekta ya Habari na Uchumi wa Vyombo vya Utangazaji

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesema utekelezaji wa mfumo...

More like this

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

Dkt. Mwigulu aweka jiwe la Msingi Mradi wa Umeme Mkata

Ni ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 60 📌Mradi...