Watu watatu wafariki kwa ajali Kimara Stop Over

Na Mwandishi Wetu

WATU watatu wafariki na wengine wamejeruhiwa kwenye ajali iliyotokea usiku wa kuamkia Februari 14,2025 katika Mtaa wa Kimara Stop Over.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema ajali imehusisha lori lililohama njia na kuparamia kituo cha bodaboda kilichopo Kimara Stop Over.

Amesema Lori hilo lilikuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam na katika ajali hiyo hadi saa 9:00 alfajiri miili mitatu iliyokuwa imekandamizwa na kontena la lori hilo imeshatolewa.

“Miili ya watu hawa inasemekana walikuwa madereva pikipiki, pia tumefanikiwa kutoa pikipiki ambazo kwa idadi ni nyingi kuliko watu tuliowakuta kwa mantiki hiyo taarifa ya Polisi itaweka bayana,” amesema Chalamila.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, RPC Mtatiro Kitinkwi amesema kutokana na idadi ya pikipiki kuwa kubwa kuliko miili iliyokutwa, inawezekana wakati wa tukio watu walikimbia kujiokoa.

“Taarifa kwa kirefu tutaitoa tukishajua chanzo cha ajali hii kwa kuwa imetokea usiku na tumekuwa hapa kwa zaidi ya saa mbili,” amesema Kamanda Kitinkwi.

Baadhi ya mashuhuda wanasema gari hilo lilifeli brake na kukwepa daladala zilizokuwa zimebaki kwenye zebra na kuangukia watu waliokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara pamoja na pikipiki 15, zilizokuwa zimeegeshwa kwenye eneo hilo.

spot_img

Latest articles

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

More like this

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...