Rais Samia kufanya ziara nchini Ethiopia, kushiriki Mkutano wa Au

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi Addis Ababa nchini Ethiopia kuanzia leo Februari 14 hadi 16 kushiriki mkutano wa kawaida wa 38 wa Nchi na serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga, imeeleza kuwa mkutano huo unatarajia kuchagua mwenyekiti mpya wa AU kwa mwaka 2025 atakayechukua nafasi ya mwenyekiti wa sasa Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania.

Pia, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo mwenyekiti, makamu mwenyekiti na makamishna sita.

“Aidha, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makamishna 6.

“Vilevile, Mkutano utajadili Taarifa ya Ushiriki wa Umoja wa Afrika kwenye Mkutano wa Nchi Tajiri Duniani (G20), Utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na Taarifa kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabianchi,” imeeleza taarifa hiyo.

Imeongeza kuwa mbali na masuala hayo, Mkutano utajadili Ajenda kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iliyopendekezwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kabla ya kushiriki Mkutano wa 38, Rais Dkt. Samia atashiriki Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika utakaofanyika Februari 14,

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...