Kesi ya DRC dhidi ya Rwanda kusikilizwa leo katika Mahakama ya haki za binadamu Arusha

Na Mwandishi Wetu

KESI iliyofunguliwa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dhidi ya Rwanda katika Mahakama ya Afrika ya haki za watu na zile za Binadamu inasikilizwa leo jijini Arusha – huku Kongo ikiishitaki Rwanda kwa kukiuka mipaka ya kimamlaka ya Kongo, kuchochea machafuko mashariki kwa Kongo na kusababisha uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.

Kesi hiyo itakayosikilizwa kwa siku mbili leo (12 Februari) na kesho (13 Februari) inahusu mapigano ya tangu Mwaka 2021, kati ya vikosi vya Kongo na waasi wa M23 ambao Kongo inadai wamekuwa wakifadhiliwa na Rwanda.

Kinshasa inadai kupitia mapigano hayo Rwanda na washirika wake wamesababisha watu zaidi ya 500,000 kukimbia makazi yao, huduma za kijamii kama hospitali na shule kufungwa na hata kusababisha watoto zaidi ya 20,000 kukosa elimu.

Madai mengine ya Kongo dhidi ya Rwanda yanahusu kuhifadhi wahalifu wa kivita bila ya kuwachukilia hatua za kisheria au kuwarudisha Kongo ili waadhibiwe kisheria.

Kwa kuileta kesi hiyo katika Mahakama hiyo ya kikanda, Kongo inatumaini mahakama hii itaitia hatiani Rwanda kwa ukiukwaji wa Mamlaka ya Mipaka ya Kiutawala ya Kongo, kuchochea machafuko na kusababisha uvunjifu mkubwa haki za binadamu.

Kwa madai hayo, Kongo inataka Mahakama iamuru Rwanda kuacha kufadhili vikundi vya waasi, kuondoa wanajeshi wake katika mipaka ya Kongo na kulipa fidia kwa waathirika wa machafuko yaliyosababishwa.

Rwanda inakanusha madai haya, na hata kutilia shaka mamlaka ya Mahakama kusikiliza kesi hiyo na inataka kesi itupiliwe mbali.

Source: BBC Swahili

spot_img

Latest articles

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

More like this

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...