Wahandisi nchini wametakiwa kufanyakazi kwa kuzingatia maadili

Na Mwandishi Wetu

WAHANDISI nchini wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, nidhamu na uwajibikaji kazini.

Wito huo umetolewa leo Februari 11, 2025 na Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Mhandisi Bernard Kavishe wakati wa semina ya 18 ya utangulizi kwa wahandisi 362 waliojiandikisha katika Mpango wa Mafunzo kwa vitendo 362 waliojiandikisha mafunzo kwa vitendo (SEAP).

Amesema semina hiyo imelenga kuwajengea msingi imara watumishi wapya ili waweze kutimiza malengo ya Bodi kwa ufanisi.

“Mafunzo haya hua tunayatoa kila mwaka, ambapo tunawaelekeza wahandisi kufanya kazi kwa kuzingatia miiko na maadili yaliyowekwa na bodi,” amesema.

Aidha amesema na kutoa mafunzo hayo pia wahandisi zaidi ya 200 wameapa kiapo cha uadilifu.

“Kwa upande wa kiapo ambacho kimefanyika leo kinahusu moyo wa kujitoa na uadilifu, na kazi ya bodi ni kuwalea wahandisi tangu pale wanapomaliza shule mpaka wanapostaafu kuhakikisha wanaendelea kujinoa na kufanya kazi kuhakikisha mambo ya taifa hili yanaenda sawa,” amesema Kavishe.

Akifungua mafunzo hayo, Msajili wa bodi ya Wahandisi (ECI) kutoka nchini India, Dkt. Priya Swarup amesema kwa miaka mingi India na Tanzania wamekuwa wakishirikiana katika mambo mbalimbali.

“Sisi ni marafiki wa muda mrefu na tutaendelea kushirikiana katika mambo mbalimbali pamoja na kuwajengea uwezo katika masuala haya ya uhandisi,” amesema Swarup.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Asha Mahimbo amesema semina hiyo itawasaidia kuwaongezea uzoefu na kujua soko lililopo nje linahitaji wahandisi wa aina gani.

“Lakini pia kuweza kuendana na sheria na taratibu za wahandisi ili mwisho wa siku tusije tukaonekana ni wahandisi ambao hatuendani na vigezo vya nchi husika,” amesema.

Aidha ametoa wito kwa wasichana kusoma masomo ya sayansi na kuacha kuyaogopa, Mhandisi Adrew Mongella ambaye ni miongoni wahandisi waliokula kiapo, amesema kiapo hicho kina maana ya kwamba unapokuwa mhandisi ni lazima uzingatie maadili yako na namna ya kuitumia taaluma yako kwaajili ya kujenga Taifa.

“Ni kiapo cha msingi kinaonesha utayari lakini pia kuzingatia maadili ya kitaaluma na sisi kama wahandisi tunao wajibu wa kujisimamia na kuzingatia miiko,” amesema Mongella.

spot_img

Latest articles

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

More like this

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...