Rais wa Malawi aagiza kuondoa majeshi yake DRC

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Malawi, Lazarus Chakwera amemuagiza Kamanda wa Jeshi la nchi hiyo kujiandaa kuondoa Majeshi ya Malawi, kutoka eneo la Mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kulingana na taarifa Televisheni ya Serikali.

Taarifa hiyo ilisema uamuzi wa Rais unalenga kuheshimu tangazo la kusitisha mapigano kati ya pande zinazozana, ingawa uamuzi wa kusitisha mapigano ulikuwa ni mpango wa waasi wa M23, ambao uliibuka baada ya kundi hilo kushambulia Nyabibwe katika Jimbo la Kivu Kusini mwa DRC.

Rais Lazarus Chakwera alikuwa chini ya shinikizo la kuondoa Majeshi ya nchi yake Mashariki mwa DRC, baada ya wanajeshi watatu wa Malawi kuuawa katika mashambulizi ya M23 mjini Goma.

Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Ujumbe wa kulinda amani wa Kusini mwa Afrika uliotumwa na SADC kusaidia mamlaka ya Congo, kukabiliana na makundi yenye silaha katika eneo la mashariki linalokabiliwa na mzozo.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...