Wataalam 2980 wajengewa uwezo kutoa huduma za afya ya akili

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kudhibiti madhara ya mmomonyoko na kupanuka kwa kingo za mito.

Khamis amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Bagamoyo Muharami Mkengealiyetaka kujua ni lini Serikali itajenga Kingo za Mto Mpiji wilayani Bagamoyo mkoani Pwani zilizopanuka kutokana na Mvua kubwa na hivyo kuhatarisha nyumba za wananchi wa maeneo hayo.

Amesema jitihada zilizofanywa na Serikali ni pamoja na kuandaa Mwongozo wa Usafishaji wa Mito ili kuondoa mchanga na tope ambapo kikosi kazi kimeundwa kwa ajili ya kushughulikia suala la usafishaji wa mito.

“Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Mazingira sura 191 kifungu cha 57 (2) kimempa Waziri mamlaka ya kutunga kanuni ndogo na mwongozo na tayari kuna hatua zimeanza kuchukuliwa kwa kufanya doria na kuzuia mali au gari litakalokutwa na kupigwa faini,” amesema Khamis.

Pamoja na hatua hiyo, Naibu Waziri Khamis ameongeza kuwa Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili watambue umuhimu wa kutunza mazingira katika mito.

Aidha, ameeleza kuwa katika kudhibiti athari za mvua, Serikali inatumia njia za asili za kudhibiti mmomonyoko wa kingo za mito kwa kupanda miche 5,000 aina ya michikichi, migomba, miti maji na matete katika kingo za mto katika eneo lenye ukubwa wa ekari 100 katika Kata ya Mabwepande wilayani Kinondoni mkoani Dar e Salaam.

spot_img

Latest articles

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

More like this

Mwigulu rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...