Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...