Rais Ruto akubali yaishe, akataa kutia saini Muswada wa Fedha

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amekataa kutia saini na ameondoa kabisa muswada wenye utata wa fedha wa mwaka 2024, ambao umesababisha maandamano na vurugu nchini kote. Rais Ruto ametoa hotuba hiyo leo Juni 26,2024 kwa taifa baada ya maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Kenya, hasa yakiongozwa na vijana waliolalamikia nyongeza mpya za ushuru wakisema zitawaongezea mzigo wa maisha.

Taarifa hii imekuja wakati waandamanaji wakiapa kuendelea na maandamano yao kupinga nyongeza hizo za ushuru, siku moja tu baada ya polisi kufyatua risasi na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 20 katika maandamano hayo yaliyogeuka kuwa vurugu.

Spika wa Bunge la Taifa, Moses Wetangula, amewasifu vijana kwa ujasiri wao, lakini amesisitiza kwamba malalamiko yao lazima yafuate mkondo wa sheria ili yapate kusikilizwa.

Katika hali nyingine, mahakama ya Eldoret imesitisha operesheni zake kwa muda baada ya waandamanaji kuharibu hati muhimu hapo jana.

spot_img

Latest articles

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

More like this

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...