Rais Ruto akubali yaishe, akataa kutia saini Muswada wa Fedha

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya, William Ruto, amekataa kutia saini na ameondoa kabisa muswada wenye utata wa fedha wa mwaka 2024, ambao umesababisha maandamano na vurugu nchini kote. Rais Ruto ametoa hotuba hiyo leo Juni 26,2024 kwa taifa baada ya maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Kenya, hasa yakiongozwa na vijana waliolalamikia nyongeza mpya za ushuru wakisema zitawaongezea mzigo wa maisha.

Taarifa hii imekuja wakati waandamanaji wakiapa kuendelea na maandamano yao kupinga nyongeza hizo za ushuru, siku moja tu baada ya polisi kufyatua risasi na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 20 katika maandamano hayo yaliyogeuka kuwa vurugu.

Spika wa Bunge la Taifa, Moses Wetangula, amewasifu vijana kwa ujasiri wao, lakini amesisitiza kwamba malalamiko yao lazima yafuate mkondo wa sheria ili yapate kusikilizwa.

Katika hali nyingine, mahakama ya Eldoret imesitisha operesheni zake kwa muda baada ya waandamanaji kuharibu hati muhimu hapo jana.

spot_img

Latest articles

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...

CRDB yashirikiana na Kids’ Holiday Festival kukuza elimu ya fedha kwa watoto

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imeingia makubaliano ya ushirikiano na Kids’ Holiday Festival...

More like this

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...