Polisi wakabiliana na waandamanaji mjini Nairobi

Nairobi, Kenya

Makabiliano makali yamezuka katikati ya mji Mkuu wa Kenya, Nairobi, baada ya polisi kuwatawanya waandamanaji wanaopinga muswada wa fedha wa 2024.

Umati wa waandamanaji ulikuwa umekusanyika katika barabara mbalimbali kupinga Muswada wa Fedha wa 2024 wakati makabiliano yalipozuka.

Polisi waliwarushia vitoa machozi waandamanaji waliokuwa wamejihami kwa maji na simu za rununu ili kueleza msimamo wao dhidi ya Muswada huo.

Umati huo ulianza kukusanyika mapema saa moja asubuhi karibu na Hifadhi ya Kitaifa ya Kenya.

Vikundi hivyo vilikuwa vikiimba kauli mbiu za pingamizi dhidi ya Muswada wa fedha huku maduka kadhaa yakisalia kufungwa katika maeneo mbalimbali ya katikati ya mji huo.

Waandalizi wa maandamano hayo, vijana ambao wanafahamika kama Gen Z wanatoa wito kwa zaidi ya watu milioni moja kujitokeza na kushiriki.

Maandamano hayo yaliyopewa jina la “Kenya Reject-Finance Bill 2024,” yamekuwa yakishika kasi na kuwavuta maelfu ya watu mitaani wiki jana kutoa upinzani wao.

Kulingana na michakato ya bunge, leo hii ni hatua ambapo wabunge hupitia Mswada kifungu kwa kifungu kinachopendekeza marekebisho katika kile kinachojulikana katika lugha ya bunge kama kamati ya bunge zima.

Muswada huo ulipita awamu ya pili wiki iliyopita baada ya wabunge 204 kuunga mkono huku 115 wakiupinga. Baada ya hapo muswada huo utasogea awamu ya tatu ambapo Bunge litaupigia kura ukiwa na marekebisho mapya.

Waandamanaji wanahoji kuwa mpango wa kukusanya kodi zinazopendekezwa za katika muswada huo zitazidisha hali ngumu ya kiuchumi kwa Wakenya wa kawaida.

Siku ya Jumatatu, serikali ilionya Wakenya wanaopanga kuandamana Jumanne dhidi ya aina yoyote ya ghasia na uharibifu wa mali.

Waziri wa Mambo ya Ndani Kithure Kindiki, mbali na kukiri kwamba kila Mkenya ana haki ya kuandamana au kulaani, alisisitiza kwamba waandamanaji hawapaswi kukiuka haki na uhuru wa wengine.

spot_img

Latest articles

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

More like this

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...