Wanafunzi 250,000 elimu ya juu kukopeshwa Sh bilioni 787

Na Nora Damian

Wanafunzi 250,000 wa vyuo vya kati na elimu ya juu wanatarajia kunufaika na mikopo katika mwaka wa masomo 2024/2025 ambapo Sh bilioni 787 zimetengwa.

Idadi hiyo ya wanafunzi imeongezeka kutoka 224,056 wa mwaka 2023/2024 ambapo watakaonufaika ni wa shahada za awali, stashahada, stashahada ya umahiri katika mafunzo ya sheria kwa vitendo, shahada za umahiri na uzamivu na ruzuku za Samia.

Akizungumza leo Juni 6,2024 wakati wa uzinduzi wa msimu mpya wa uombaji mikopo Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Dk. Bill Kiwia, amesema dirisha la kuomba mikopo kwa njia ya mtandao litakuwa wazi kwa siku 90 hadi Agosti 31,2024 na kusisitiza kuwa hawataongeza muda.

“Kwa uzoefu wetu siku 90 zinatosha kwa kuwa mwombaji akiwa amejiandaa na nyaraka zote muhimu inamchukua muda wa dakika 40 kukamilisha maombi yake kwa njia ya mtandao. Hivyo, tunasisitiza waombaji wa mikopo kuzingatia muda uliotolewa kwa kuwa hatutarajii kuongeza baada ya Agosti 31,” amesema Dk. Kiwia.

Amesema pia mwombaji atapaswa kuwa na akaunti ya benki na kwamba kwa waombaji wenye namba za nida watapaswa kuziweka wakati wa kuomba mkopo na kama mwombaji hana anaweza kuendelea na maombi bila namba hiyo.

Mkurugenzi huyo amesisitiza wanafunzi wanaoomba mkopo kusoma na kuzingatia maelekezo yaliyomo katika miongozo ya utoaji mikopo na ruzuku ambayo tayari imewekwa kwenye tovuti ya bodi hiyo ikiwa katika lugha za Kiswahili na Kiingereza.

spot_img

Latest articles

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

More like this

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

Jessica: CCM inajali uongozi wa vijana

Na Mwandishi Wetu KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA, Jessica Mshama...

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...