Doyo kugombea uenyekiti ADC, amkaribisha Mchungaji Msigwa

Na Winfrida Mtoi

Katibu Mkuu wa Chama cha  Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho Taifa baada ya Hamad Rashid Mohammed kumaliza muda wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6, 2024 jijini Dar es Salaam, Doyo amesema anatangaza kugombea nafasi hiyo kwa kuamini  ana uwezo wa kukitumikia chama hicho katika kutekeleza matakwa ya Katiba.

“Mimi nimejipanga kuwa mwenyekiti wa chama hiki ili kurithi mikoba ya Mheshimiwa  Hamadi Rashid kwa sababu  nimepata mafunzo makubwa sana kutoka kwake. Huyu ni mwanasiasa mzoefu na amefanya kazi na wanasiasa wakongwe,” amesema Doyo.

Amesema Hamad amewafunza jambo katika chama hicho kwani ameonyesha kufuata matakwa ya Katiba kwa  kuachia ngazi baada ya kumaliza muda wake na kuwapa funzo vijana wa chama hicho na wana siasa wengine nchini.

Doyo ameeleza kuwa kati ya mafunzo aliyopata kutoka kwa mwanasiasa huyo mkongwe ni uvumilivu na kupambana na kila changamoto.

Katika hatua nyingine, amemkaribisha Mchungaji Peter  Msigwa wa  Chadema kujiunga na chama hicho endapo haridhishwi na mambo yanavyokwenda huko aliko.

spot_img

Latest articles

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...

‘Uandishi wa kidijitali ndiyo mpango mzima’

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya Media Brains ikishirikiana na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

More like this

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUFUFUA SKIMU YA MATIPWILI

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema iko tayari kufufua na kuboresha skimu ya Umwagiliaji Matipwili...

Tanzania, AngloGold Ashanti kuimarisha ushirikiano

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na ujumbe wa kampuni ya...

TANESCO YABAINI MATUKIO YA WIZI WA UMEME KINONDONI KASKAZINI

📌 Operesheni ya ukaguzi wa mita yabaini matumizi yasiyo halali ya umeme eneo la...