Rais Yanga awatoa hofu mashabiki

Na Winfrida Mtoi

Uongozi wa Klabu ya Yanga umewatoa hofu wadau wa timu hiyo kuwa itaendelea kufanya vizuri kwa kuahidi kuwabakiza wachezaji wote inaowahutaji na kuongeza wengine kuimarisha kikosi.

Hayo yamesemwa na Rais wa klabu hiyo,  Hersi Saidi leo Juni 5, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa pamoja na kupata mafanikio makubwa msimu huu, wanajipanga kufanya vizuri zaidi msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine.

Ameeleza kuwa mafanikio ya msimu huu yametokana na kujitoa kwa dhati kwa wachezaji wao na uongozi mzima wa benchi la ufundi.

“Niwapongeze wachezaji wetu, kazi kubwa mmeifanya, Kuanzia leo tunawapa wachezaji wetu likizo ya mwezi mmoja, tutakutana nao tena mwanzoni mwa mwezi wa saba wa  kujiandaa na msimu mpya ambapo tutakuwa tayari tumefanya usajili wa kuimarisha kikosi chetu,” amesema Hersi.

Msimu huu Yanga imefanikiwa  kutetea mataji yake mawili la Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la TFF, huku michuano ya Kimataifa ikifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

spot_img

Latest articles

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

More like this

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...