Rais Yanga awatoa hofu mashabiki

Na Winfrida Mtoi

Uongozi wa Klabu ya Yanga umewatoa hofu wadau wa timu hiyo kuwa itaendelea kufanya vizuri kwa kuahidi kuwabakiza wachezaji wote inaowahutaji na kuongeza wengine kuimarisha kikosi.

Hayo yamesemwa na Rais wa klabu hiyo,  Hersi Saidi leo Juni 5, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa pamoja na kupata mafanikio makubwa msimu huu, wanajipanga kufanya vizuri zaidi msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine.

Ameeleza kuwa mafanikio ya msimu huu yametokana na kujitoa kwa dhati kwa wachezaji wao na uongozi mzima wa benchi la ufundi.

“Niwapongeze wachezaji wetu, kazi kubwa mmeifanya, Kuanzia leo tunawapa wachezaji wetu likizo ya mwezi mmoja, tutakutana nao tena mwanzoni mwa mwezi wa saba wa  kujiandaa na msimu mpya ambapo tutakuwa tayari tumefanya usajili wa kuimarisha kikosi chetu,” amesema Hersi.

Msimu huu Yanga imefanikiwa  kutetea mataji yake mawili la Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la TFF, huku michuano ya Kimataifa ikifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

spot_img

Latest articles

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

More like this

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...