Rais Yanga awatoa hofu mashabiki

Na Winfrida Mtoi

Uongozi wa Klabu ya Yanga umewatoa hofu wadau wa timu hiyo kuwa itaendelea kufanya vizuri kwa kuahidi kuwabakiza wachezaji wote inaowahutaji na kuongeza wengine kuimarisha kikosi.

Hayo yamesemwa na Rais wa klabu hiyo,  Hersi Saidi leo Juni 5, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa pamoja na kupata mafanikio makubwa msimu huu, wanajipanga kufanya vizuri zaidi msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine.

Ameeleza kuwa mafanikio ya msimu huu yametokana na kujitoa kwa dhati kwa wachezaji wao na uongozi mzima wa benchi la ufundi.

“Niwapongeze wachezaji wetu, kazi kubwa mmeifanya, Kuanzia leo tunawapa wachezaji wetu likizo ya mwezi mmoja, tutakutana nao tena mwanzoni mwa mwezi wa saba wa  kujiandaa na msimu mpya ambapo tutakuwa tayari tumefanya usajili wa kuimarisha kikosi chetu,” amesema Hersi.

Msimu huu Yanga imefanikiwa  kutetea mataji yake mawili la Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la TFF, huku michuano ya Kimataifa ikifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

spot_img

Latest articles

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...

More like this

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...