Rais Yanga awatoa hofu mashabiki

Na Winfrida Mtoi

Uongozi wa Klabu ya Yanga umewatoa hofu wadau wa timu hiyo kuwa itaendelea kufanya vizuri kwa kuahidi kuwabakiza wachezaji wote inaowahutaji na kuongeza wengine kuimarisha kikosi.

Hayo yamesemwa na Rais wa klabu hiyo,  Hersi Saidi leo Juni 5, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa pamoja na kupata mafanikio makubwa msimu huu, wanajipanga kufanya vizuri zaidi msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Mabingwa Afrika na michuano mingine.

Ameeleza kuwa mafanikio ya msimu huu yametokana na kujitoa kwa dhati kwa wachezaji wao na uongozi mzima wa benchi la ufundi.

“Niwapongeze wachezaji wetu, kazi kubwa mmeifanya, Kuanzia leo tunawapa wachezaji wetu likizo ya mwezi mmoja, tutakutana nao tena mwanzoni mwa mwezi wa saba wa  kujiandaa na msimu mpya ambapo tutakuwa tayari tumefanya usajili wa kuimarisha kikosi chetu,” amesema Hersi.

Msimu huu Yanga imefanikiwa  kutetea mataji yake mawili la Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho la TFF, huku michuano ya Kimataifa ikifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

spot_img

Latest articles

Elimu ya Nishati safi ya kupikia yawafikia maafisa dawati ngazi ya mikoa na Halmashauri

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati imeanza kutoa elimu kuhusu Nishati Safi ya Kupikia...

Jaji Mwambegele Akagua Maandalizi ya Vituo Maalum vya Kupigia Kura Wilayani Tanganyika

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa...

Simba nayo yaenda hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika

Na Winfrida Mtoi Mabao ya ugenini yameibeba Simba kwenda makundi Ligi ya Mabingwa Afrika baada...

Mrindoko: Mradi wa TACTIC utanufaisha wananchi wa Mpanda

Na Mwandishi wetu, Katavi MKUU wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, amesema utekelezaji wa Mradi...

More like this

Elimu ya Nishati safi ya kupikia yawafikia maafisa dawati ngazi ya mikoa na Halmashauri

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati imeanza kutoa elimu kuhusu Nishati Safi ya Kupikia...

Jaji Mwambegele Akagua Maandalizi ya Vituo Maalum vya Kupigia Kura Wilayani Tanganyika

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa...

Simba nayo yaenda hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika

Na Winfrida Mtoi Mabao ya ugenini yameibeba Simba kwenda makundi Ligi ya Mabingwa Afrika baada...