Twaha Kiduku atamba yupo fiti kumkabili mhindi

Na Winfrida Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Twaha Kiduku leo Aprili 3,2024 amewaongoza mabondia wenzake mkoani Morogoro kupima afya kuelekea pambano lake dhidi ya Hapreet Sight kutoka India.

Pambano hilo la Kimataifa lisilokuwa la ubingwa lililopewa jina la ‘Hatukimbii Hatuogopi’ linatarajia kupigwa siku ya Idd Pili kwenye ukumbi wa Tanzanite, mkoani Morogoro.

Akizungumzia maandalizi yake, Kiduku amesema amekamilisha kwa asilimia kubwa na yupo tayari kuliwakilisha vizuri Taifa kwa kuibuka na ushindi.

“Mimi pamoja na timu yangu tuko vizuri kiafya na kila kitu, naamini siwezi kuwaangusha Watanzania. Hakuna ugomvi rahisi, siku zote ugomvi ni ugomvi kikubwa ni kujiandaa na kumheshimu mpinzani,” amesema Kiduku.

Mara ya mwisho Kiduku alipanda ulingoni Desemba mwaka jana na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhindi ya Mganda, Mohammed Sebyala, jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mratibu wa Habari wa Peak Time ambao ni waandaaji wa pambano hilo, Victor Denis amesema kwa sasa kilichobaki ni mashabiki kuona burudani ya masumbwi kutokana na kila bondia kuwa fiti.

Mabondia wengine watakaozichapa siku hiyo ni Karim Mandonga dhidi ya Mada Maugo,Jamali Kunoga wa Marogoro kuchapana na Mrisho Mzezele wa Mbagala Dar es Salaam na mapambano mengine mengi.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...