Twaha Kiduku atamba yupo fiti kumkabili mhindi

Na Winfrida Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Twaha Kiduku leo Aprili 3,2024 amewaongoza mabondia wenzake mkoani Morogoro kupima afya kuelekea pambano lake dhidi ya Hapreet Sight kutoka India.

Pambano hilo la Kimataifa lisilokuwa la ubingwa lililopewa jina la ‘Hatukimbii Hatuogopi’ linatarajia kupigwa siku ya Idd Pili kwenye ukumbi wa Tanzanite, mkoani Morogoro.

Akizungumzia maandalizi yake, Kiduku amesema amekamilisha kwa asilimia kubwa na yupo tayari kuliwakilisha vizuri Taifa kwa kuibuka na ushindi.

“Mimi pamoja na timu yangu tuko vizuri kiafya na kila kitu, naamini siwezi kuwaangusha Watanzania. Hakuna ugomvi rahisi, siku zote ugomvi ni ugomvi kikubwa ni kujiandaa na kumheshimu mpinzani,” amesema Kiduku.

Mara ya mwisho Kiduku alipanda ulingoni Desemba mwaka jana na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhindi ya Mganda, Mohammed Sebyala, jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mratibu wa Habari wa Peak Time ambao ni waandaaji wa pambano hilo, Victor Denis amesema kwa sasa kilichobaki ni mashabiki kuona burudani ya masumbwi kutokana na kila bondia kuwa fiti.

Mabondia wengine watakaozichapa siku hiyo ni Karim Mandonga dhidi ya Mada Maugo,Jamali Kunoga wa Marogoro kuchapana na Mrisho Mzezele wa Mbagala Dar es Salaam na mapambano mengine mengi.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...