Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu

TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, inatarajiwa kuwasilisha ripoti yake rasmi kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Aprili 23, 2026.

Taarifa kukabidhi ripoti hiyo imetolewa leo Aprili 21, 2026 Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Othman Chande, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Tume.

Jaji Chande amesema jumla ya watu 63,603 wameifikia tume hiyo kutoa ushahidi wao kwa njia mbalimbali, ikiwemo kukutana ana kwa ana, kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi na dodoso.

Amefafanua kuwa idadi kubwa ya ushahidi imepokelewa kupitia njia ya simu na ujumbe mfupi, ambapo watu 56,445 waliwasilisha taarifa zao kwa njia hiyo, watu 1,323, mashihidi wa viapo (Affidavit) watu 553, madodoso yenye maswali bila mtu kutaja jina lake ni 4, 891 na mikutano na makundi 202

Amesema kazi ya Tume hiyo imehusisha ukusanyaji wa ushahidi, maoni ya wadau mbalimbali pamoja na uchambuzi wa kina wa taarifa zilizokusanywa, ili kuhakikisha kuwa ripoti inayowasilishwa inakuwa ya kuaminika na yenye manufaa kwa Taifa.

Amesema ripoti hiyo itakayotolewa inatarajiwa kuwekwa hadharani kwa sababu ya maslahi ya umma na kuwezesha watu waone uhalisi wa nini kilitokea.

Tume hiyo ilizinduliwa Novemba 20, 2025 na Rais Samia kuchunguza undani wa sababu na chanzo cha matukio ya maandamano yaliyozaa vurugu siku ya Uchaguzi Mkuu.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...