SEHEMU YA NCHI GIZANI

Sehemu kadhaa nchini zimekumbwa na ‘giza’ kwa saa kadhaa leo Jumatatu Machi 4, 2024, baada ya umeme kukatika kutokana na kile ambacho Shirika la Umeme Tanzania [TANESCO] limekitaja kuwa ni hitilafu iliyotokea katika gridi ya Taifa.

Taarifa iliyotolewa na Tanesco imesema hitilafu hiyo ingesababisha kukosekana kwa umeme kwa baadhi ya maeneo ya Tanzania Bara na Zanzibar.”Shirika linawaomba radhi kwa usumbufu wowote utakao jitokeza”, inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Kwa upande mwingine, Mtandao wa Millardayo umelinukuu Shirika la Umeme Zanzibar [ZECO] likisema Zanzibar nzima imekosa umeme kuanzia saa 7 mchana wa leo kutokana na hitilafu iliyotokea Tegeta, Dar es Salaam.

“Mpendwa mteja kuna hitilafu ya umeme mkubwa mkondo wa kilovolti 132 kutoka Tegeta Bara kuja Zanzibar kuliko sababisha kuzimika umeme hafla maeneneo yote ya Zanzibar. Zeco inaomba radhi kwa usumbufu unaoendelea kujitokeza ahsante,” ZECO

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...