Watalii waongezeka Kilwa

Na Mwandishi wetu, Kilwa

Idadi ya watalii kutoka Mataifa mbalimbali duniani imezidi kuongezeka katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kutokana na utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA ),taasisi yenye dhamana ya usimamizi wa hifadhi hiyo, Februari 15,2024 ilipokea kundi la tani la watalii 119 kutoka ikiwa ni mfululizo wa safari za watalii wa nje kutembelea hifadhi hiyo kwa shughuli za utalii.

Watalii waliowasili ni kutoka katika nchi za Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ubelgiji, Hispania na Canada wakisafirishwa na meli iitwayo Le Bougainville.

Kwa mujibu wa TAWA, hayo ni matokeo ya hatua za makusudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha sekta ya utalii nchini inakua kwa kasi baada ya kucheza filamu maarufu iitwayo Tanzania The Royal Tour.

Pia jitihada za dhati zilizofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka hiyo kwa kuboresha miundombinu wezeshi ya utalii katika hifadhi hiyo.

spot_img

Latest articles

CHELSEA BINGWA WA FIFA CWC 2025

Timu ya Chelsea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Klabu kwa kuchapa...

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...

Ndumbaro: Sheria 300 Zimetafsiriwa kwa Kiswahili Ili Kuimarisha Uelewa kwa Wananchi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema kuwa hadi...

More like this

CHELSEA BINGWA WA FIFA CWC 2025

Timu ya Chelsea imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Klabu kwa kuchapa...

Humphrey Polepole ajiuzulu

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubalozi na...

Nandy ahamasika kutangaza Nembo ya Made in Tanzania Kimataifa

Na Tatu Mohamed MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Faustina Mfinanga (Nandy), amesema elimu aliyoipata...