Watalii waongezeka Kilwa

Na Mwandishi wetu, Kilwa

Idadi ya watalii kutoka Mataifa mbalimbali duniani imezidi kuongezeka katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kutokana na utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA ),taasisi yenye dhamana ya usimamizi wa hifadhi hiyo, Februari 15,2024 ilipokea kundi la tani la watalii 119 kutoka ikiwa ni mfululizo wa safari za watalii wa nje kutembelea hifadhi hiyo kwa shughuli za utalii.

Watalii waliowasili ni kutoka katika nchi za Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ubelgiji, Hispania na Canada wakisafirishwa na meli iitwayo Le Bougainville.

Kwa mujibu wa TAWA, hayo ni matokeo ya hatua za makusudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha sekta ya utalii nchini inakua kwa kasi baada ya kucheza filamu maarufu iitwayo Tanzania The Royal Tour.

Pia jitihada za dhati zilizofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka hiyo kwa kuboresha miundombinu wezeshi ya utalii katika hifadhi hiyo.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...