Tano za Yanga zamng’oa kocha Simba

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

UONGOZI wa klabu ya Simba umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa kikosi hicho, Robertinho Oliveira kwa kuvunja mkataba wake wa miaka miwili aliotumikia kwa kipindi cha miezi 10.

Kocha huyo anaondoshwa ikiwa ni siku mbili tu baada ya kufungwa na watani zao Yanga mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Jumapili Novemba 5, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho raia wa Brazil, alijiunga na Simba Januari 3, 2023 akitokea Vipers SC ya Uganda na ameiongoza Simba katika michezo zaidi ya 25, ya Ligi Kuu Tanzania Bata na Kimataifa.

Katika Ligi Kuu tangu ametua nchini, amecheza mechi 18, akipoteza moja pekee dhidi ya Yanga huku akitoka sare mbili, huku akiipa Simba taji la Ngao ya Jamii alilotwaa msimu huu baada ya Wanamsimbazi hao kulikosa kwa misimu miwili mfululizo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba, pia imefikia makubaliano ya kusitisha mkataba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.

“Katika kipindi cha mpito kikosi chetu kitakuwa chini ya kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Selemani Matola. Tayari mchakato wa kutafuta makocha wapya umeanza na unatarajiwa kukamilika hivi  punde,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

More like this

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...