Mashambulizi Israel| Watanzania wawili hawajulikani walipo

*Ni wanafunzi, Ubalozi waeleza

Yerusalemu, Israel

Ubalozi wa Tanzania nchini Israel unasema kuwa hauna mawasiliano naWatanzania wawili ambao wanakaa eneo la kusini ambalo limeshuhudia mapambano baina ya wanamgambo wa Kipalestina wa Hamas na jeshi la Israeli.

Balozi wa Tanzania nchini Israel, Alex Kallua amelielezwa Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC) mapema leo Oktoba 9, kuwa mpaka leo asubuhi, ubalozi huo umekuwa na mawasiliano na Watanzania takribani 350 waliopo nchini humo kasoro wanafunzi hao wawili.

Balozi Kallua amesema: ”Tunaendelea kuwafuatilia Watanzania wawili ambao ni wanafunzi waliokuwa wanafanya mafunzo kwa vitendo ‘internship’ kusini mwa nchi hiyo. Tunafanya jitihada za kuwapata kwanza ili kufahamu walipo na hali zao.…wanafunzi wengine takribani 260 kati ya Watanzania zaidi ya 350 wako salama katika maeneo mbalimbali nchini humo na wamekuwa na mawasiliano na ubalozi,” amesema Balozi huyo.

Sambamba na hayo, balozi huyo amesema kuwa wanaendelea kufuatilia hali ya usalama nchini humo ili kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa salama.

”Tunafuatilia kwa karibu, na tunaendelea kupata taarifa kutoka Mamlaka za Israel kuhusu hali ilivyo. Tunaendelea kufuatilia na kuwaeleza waliopo hali ilivyo,” amesema balozi huyo.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...