Tumedunguwa ndege 29 zisizo na rubani za Urusi-Ukraine

Kiev, Ukraine

Ukraine imesema leo Jumanne Oktoba 3, kuwa imezidunguwa takribani ndege 29 zisizo na rubani zilizotengenezwa na Iran pamoja na kombora la masafa marefu lililorushwa na vikosi vya Urusi kutoka Rasi ya Crimea.

Jeshi la anga la Ukraine limesema kuwa usiku wa kuamkia leo, washambuliaji wa Urusi katika eneo hilo la Crimea, waliishambulia nchi hiyo kwa kutumia ndege hizo zisizo na rubani na kombora aina ya Iskander-K.

Taarifa ya jeshi hilo imeeleza kuwa udunguaji huo ulifanywa na vikosi vinavyohusika na eneo la kusini la Mykolaiv na eneo la kati la Dnipropetrovsk.

Ukraine yaonya

Ukraine imeonya kuwa Urusi inaanzisha upya kampeni ya mashambulizi ya anga dhidi ya miundombinu ya nishati ya Ukraine ambayo kwenye majira ya baridi kali ya mwaka jana yaliwaacha mamilioni ya watu bila gesi ya kupashia joto nyumba zao na maji kwa muda mrefu.

Wiki hii, Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine aliuhimiza Umoja wa Ulaya kuongeza vikwazo vyake dhidi ya Urusi na pia Iran kwa kupeleka ndege zake zisizo na rubani nchini Urusi.

Shirika la habari la serikali ya Urusi, RIA, limemnukuu Waziri wa Ulinzi wa Urusi, Sergei Shoigu, akisema kuwa jeshi la nchi hiyo halina mipango ya kuwahamasisha wanaume zaidi kujiunga katika vita vya Ukraine kwa sababu lina maafisa wa kutosha.

Katika hatua nyingine, wakati wa taarifa zake za kila siku kuhusu vita vya Ukraine, Wizara ya Ulinzi ya Uingereza imesema kuwa kura ya maoni iliyofanywa hivi karibuni na kituo cha serikali cha utafiti wa maoni ya umma iligundua kuwa asilimia 61 ya wale waliohojiwa wanachukulia neno “mawakala wa kigeni” kuwa wasaliti wanaoeneza uwongo kuhusu Urusi.

spot_img

Latest articles

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...

Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini 📌 Apongeza utoaji wa mafunzo...

More like this

Baraza la saba la Wafanyakazi Wizara ya Nishati lakutana Dodoma

📌 Dkt. Kazungu asema Wizara itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Kimkakati 📌 Baraza lapitisha rasimu...

Wizara ya Nishati yataja mafanikio utekelezaji majukumu 2024/25

📌 Uzalishaji umeme waongezeka kwa asilimia 59.9 📌 Misheni 300 kuongeza upatikanaji umeme...

Gavana Tutuba: Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea kuimarika

Na Tatu Mohamed GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba amesema kuwa, hali...