Sheikh Jalala ataka mabadiliko mwaka mpya wa Kiislamu

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa kuendelea kuenzi umoja na mshikamano wa kitaifa katika mwaka mpya wa Kiislamu 1445.

Mwaka Mpya wa Kiislamu ni siku muhimu katika kalenda ya Kiislamu duniani kote na huadhimishwa kila mwaka.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam Julai 18,2023 na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnashaari, Hemed Jalala, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwaka mpya wa Kiislamu.

Amewataka waislamu wajitathmini mwaka uliopita wapi wamefanikiwa, walikokwama na namna watakavyoweza kusonga mbele.

Sheikh Jalala pia amesisitiza mwaka mpya wa kiislamu uwe wa kuenzi umoja wa Watanzania wote bila kujali tofauti zao na dini zao.

“Mwaka 1445 uwe ni mwaka wa umoja, mshikamano, tuungane na kuwa kitu kimoja na kuhimiza umoja. Waislamu umefika muda wa kuacha tofauti zetu na kukaa meza moja.

“Umoja wa Watanzania ni muhimu mno, umoja wa kitaifa, kupenda Tanzania yetu ni moja kati ya misingi muhimu. Tuhubiri umoja kati ya sisi waislamu na ndugu zetu wakristo, tuhakikishe dini hizi zinashikamana, zinakaa vizuri na zinapendana,” amesema Sheikh Jalala.

Amewahimiza viongozi wa dini kuhubiri zaidi kuhusu mmomonyoko wa maadili ili vijana wawe na maadili mema yanayompendeza Mungu.

Waislamu wanasherehekea mwaka mpya wakimkumbuka pia Imamu Hussein ambaye aliuawa akipigania kurudisha maadili, mshikamano, umoja na amani katika jamii.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...