Sheikh Jalala ataka mabadiliko mwaka mpya wa Kiislamu

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa kuendelea kuenzi umoja na mshikamano wa kitaifa katika mwaka mpya wa Kiislamu 1445.

Mwaka Mpya wa Kiislamu ni siku muhimu katika kalenda ya Kiislamu duniani kote na huadhimishwa kila mwaka.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam Julai 18,2023 na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnashaari, Hemed Jalala, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwaka mpya wa Kiislamu.

Amewataka waislamu wajitathmini mwaka uliopita wapi wamefanikiwa, walikokwama na namna watakavyoweza kusonga mbele.

Sheikh Jalala pia amesisitiza mwaka mpya wa kiislamu uwe wa kuenzi umoja wa Watanzania wote bila kujali tofauti zao na dini zao.

“Mwaka 1445 uwe ni mwaka wa umoja, mshikamano, tuungane na kuwa kitu kimoja na kuhimiza umoja. Waislamu umefika muda wa kuacha tofauti zetu na kukaa meza moja.

“Umoja wa Watanzania ni muhimu mno, umoja wa kitaifa, kupenda Tanzania yetu ni moja kati ya misingi muhimu. Tuhubiri umoja kati ya sisi waislamu na ndugu zetu wakristo, tuhakikishe dini hizi zinashikamana, zinakaa vizuri na zinapendana,” amesema Sheikh Jalala.

Amewahimiza viongozi wa dini kuhubiri zaidi kuhusu mmomonyoko wa maadili ili vijana wawe na maadili mema yanayompendeza Mungu.

Waislamu wanasherehekea mwaka mpya wakimkumbuka pia Imamu Hussein ambaye aliuawa akipigania kurudisha maadili, mshikamano, umoja na amani katika jamii.

spot_img

Latest articles

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

More like this

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...