Sheikh Jalala ataka mabadiliko mwaka mpya wa Kiislamu

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa kuendelea kuenzi umoja na mshikamano wa kitaifa katika mwaka mpya wa Kiislamu 1445.

Mwaka Mpya wa Kiislamu ni siku muhimu katika kalenda ya Kiislamu duniani kote na huadhimishwa kila mwaka.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam Julai 18,2023 na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnashaari, Hemed Jalala, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mwaka mpya wa Kiislamu.

Amewataka waislamu wajitathmini mwaka uliopita wapi wamefanikiwa, walikokwama na namna watakavyoweza kusonga mbele.

Sheikh Jalala pia amesisitiza mwaka mpya wa kiislamu uwe wa kuenzi umoja wa Watanzania wote bila kujali tofauti zao na dini zao.

“Mwaka 1445 uwe ni mwaka wa umoja, mshikamano, tuungane na kuwa kitu kimoja na kuhimiza umoja. Waislamu umefika muda wa kuacha tofauti zetu na kukaa meza moja.

“Umoja wa Watanzania ni muhimu mno, umoja wa kitaifa, kupenda Tanzania yetu ni moja kati ya misingi muhimu. Tuhubiri umoja kati ya sisi waislamu na ndugu zetu wakristo, tuhakikishe dini hizi zinashikamana, zinakaa vizuri na zinapendana,” amesema Sheikh Jalala.

Amewahimiza viongozi wa dini kuhubiri zaidi kuhusu mmomonyoko wa maadili ili vijana wawe na maadili mema yanayompendeza Mungu.

Waislamu wanasherehekea mwaka mpya wakimkumbuka pia Imamu Hussein ambaye aliuawa akipigania kurudisha maadili, mshikamano, umoja na amani katika jamii.

spot_img

Latest articles

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...

Tume yataja idadi waliopoteza maisha matukio ya Oktoba 29, Dar yaongoza

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na...

More like this

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...