Papa Francis akutana na Rais Samia

Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan huku wakieleza dhamira yao ya pamoja ya kuhimiza amani duniani.

Baba Mtakatifu Francisko amempokea Rais Samia na ujumbe, mjini Vatican siku ya Jumatatu. Baada ya kukutana na Baba Mtakatifu Francisko, Rais amekutana na Katibu wa Jimbo la Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Katibu wa Vatican anayeshughulikia Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, Askofu Mkuu, Paul Richard Gallagher.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi Rasmi ya Mawasiliano ya Vatican (Holy See Press Office), viongozi hao wawili walikuwa na mjadala mzuri ambao pamoja na mambo mengine umeangazia uhusiano mwema uliopo kati ya Tanzania na Vatican.

Kadhalika wamezungumzia “mchango muhimu ambao Kanisa Katoliki limekuwa likitoa nchini Tanzania hasa katika sekta za elimu na afya. Kadhalika wamezungumzia hali ya kikanda na mambo ya sasa ya kimataifa, na pande zote mbili zilielezea matakwa yao ya pamoja ya kuhimiza amani.

Chanzo: Vatican Radio

spot_img

Latest articles

JAB yawafungia watangazaji wanne wa kipindi cha Genge la GEN TOK kwa kukiuka maadili

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewafungia...

Madai ya dada wa Polepole kubebwa, Polisi yachunguza 

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema limepokea taarifa za...

Kiungo Moussa  Conte rasmi atambulishwa Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Tanzania, Klabu ya Yanga...

Tanzania kuwa na mashirika ya umma yenye ushindani ifikapo 2050

Na Mwandishi Wetu IFIKAPO mwaka 2050, Tanzania inajiona kuwa na Mashirika ya umma ya...

More like this

JAB yawafungia watangazaji wanne wa kipindi cha Genge la GEN TOK kwa kukiuka maadili

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewafungia...

Madai ya dada wa Polepole kubebwa, Polisi yachunguza 

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema limepokea taarifa za...

Kiungo Moussa  Conte rasmi atambulishwa Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Tanzania, Klabu ya Yanga...