Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu

TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa Magereza Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Jumanne, Februari 10, 2025 kwenye dimba la Sokoine, Mbeya.

Mabao ya Coastal Union yalifungwa na Bakari Msimu dakika ya 1, 51, Shiza Kichuya dakika  ya 42, na  Cleopache Mkandala dakika ya 90+, huku bao la kufutia machozi  la Prisons likifungwa na  George Mpole dakika ya 45.

Kwa matokeo  hali bado ni mbaya kwa Tanzania Prisons iliyopo nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi tisa. Kwa upande wao, Coastal Union imefikisha pointi 14, ikipanda hadi nafasi ya tisa kutoka nafasi ya 13.

Kocha Msaidizi wa Prisons, Innocent Mwamgonde amesema waliingia uwanjani kwa lengo la kushinda mechi lakini umakini wa wachezaji haukuwa mzuri na  wapinzani wao walifanikiwa kutumia makosa waliyofanya na kupata ushindi.

Naye Kocha Mkuu wa Coastal Union, Mohammed Muya amesema ushindi huo ni zawadi ya  uvumilivu wa viongozi na mashabiki wao kwani walipitia kipindi kigumu  cha kukosa matokeo mazuri.

Pamba yatakata Mwanza

Katika mchezo mwingine, Pamba Jiji imeibuka na  ushindi nyumbani wa bao 1-0 dhidi Namungo  kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Bao hilo likifungwa na Methew Momanyi dakika ya 53.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...