Rais Samia kuongoza mazishi ya Lowassa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuongoza mazishi ya Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Lowassa yanayotarajiwa kufanyika Wilayani Monduli Mkoani Arusha Jumamosi Februari17, 2024.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema leo (Jumapilii, Februari 11, 2024) kuwa, kabla ya mazishi hayo mwili wa Hayati Lowassa unatarajiwa kuagwa katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Akitoa taarifa ya ratiba ya mazishi ya kiongozi huyo katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu Oysterbay, Dar esSalaam, Majaliwa amesema Jumanne Februari 13, 2024 mwili wa Hayati Lowasa unataangwa na viongozi na wananchi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Jumatano Februari 14 mwili wa Hayari Lowasa utapelekwa katika Kanisa la KKKT Azania Front kwa ajili ya ibada takatifu na kuaga na Alhamisi Februari 15 mwili wa Hayati Lowassa utasafirishwa kwenda jijini Arusha ambako viongozi na wananchi watapa fursa ya kuaga katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid.

Majaliwa amesema katika kipindi cha siku tano za maombolezo, Taifa litaendelea na shughuli za umma na kijamii sambamba na kushirikiana na wanafamilia katika ratiba ya msiba kama ilivyoandaliwa na kamati ya mazishi ya Kitaifa na wanafamilia.

Lowassa alifariki jana (Jumamosi, Februari 10, 2024) wakati akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam na tangazo la kifo chake lilitolewa na Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango.

Tayari Rais Samia alishatangaza siku tano za maombolezo ya kitaifa ambapo bendera zitapeperushwa nusu mlingoti kuanzia tarehe 10 Februari, 2024.

spot_img

Latest articles

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...

Tume yataja idadi waliopoteza maisha matukio ya Oktoba 29, Dar yaongoza

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na...

More like this

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...