Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu

DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho, imefanyika leo Aprili 17, 2026, jijini Dar es Salaam, ambapo Simba imepangwa dhidi ya TRA United huku Yanga ikipewa JKT Tanzania.

Kwa upande wa Azam FC watakuwa wageni, Mashujaa FC katika dimba la Lake Tanganyika, wakati Singida Black Stars itakutana na  Coastal Union  kwenye Uwanja wa  Mkwakwani, Tanga.

Akizungumzia ratiba hiyo, Ofisa Habari wa JKT Tanzania, Masau Bwire ametamba kuwa  hawaihofii kupangwa na Yanga na wamefurahia, anaamini malengo yao yatatimia ya kufika fainali baada ya msimu uliopita kuishia nusu fainali.

“Mechi yetu ya mwisho na Yanga pale KMC yaliwashitua wengi, kuwaonesha ya kwamba sisi tuko vizuri kuliko Yanga, tunakwenda kuwaonesha Watanzania, hadi hapa mechi na Yanga tushamaliza. Nina hakika kichapo cha kizalendo kitaonekana,” amesema. Masau.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...