Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu

KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, akichukua nafasi ya Mohamed Laizer ambaye amefutwa kazi kutokana na mwenendo usioridhisha wa timu.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo, Minziro ataongoza benchi la ufundi akisaidiwa na makocha  wengine Mathias Wandiba pamoja na Abubakari Francis, ambaye anaendelea na majukumu yake ndani ya kikosi hicho.

Minziro anapewa jukumu hilo wakati Fountain Gate ikiwa katika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kucheza michezo 17 na kujikusanyia alama 16.

Uongozi wa klabu hiyo umesema  una Imani na Minziro kutokana na uzoefu wake katika soka la Tanzania, huku ikiendelea kuhakikisha inajenga timu imara.

spot_img

Latest articles

Sowah apigwa faini nzito  kwa utovu wa nidhamu, ashushwa U-20

Na Winfrida Mtoi UONGOZI wa Klabu ya Simba umeweka wazi hatua kali za kinidhamu zilizochukuliwa...

Waziri Mavunde aelekeza kusimamishwa kwa shughuli za uchimbaji Busulwangili-Kahama – Kahama

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza kusimamishwa mara moja kwa...

DC Mkude akabidhi vyombo vya usafiri Tanesco Mkoa wa Arusha kuimarisha utoaji huduma

📌 Ni katika muendelezo wa mkakati wa TANESCO wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi. 📌...

DCEA yakamata Kilo 101.2 za Mirungi ndani ya Basi la Abood, watano mbaroni

Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata...

More like this

Sowah apigwa faini nzito  kwa utovu wa nidhamu, ashushwa U-20

Na Winfrida Mtoi UONGOZI wa Klabu ya Simba umeweka wazi hatua kali za kinidhamu zilizochukuliwa...

Waziri Mavunde aelekeza kusimamishwa kwa shughuli za uchimbaji Busulwangili-Kahama – Kahama

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza kusimamishwa mara moja kwa...

DC Mkude akabidhi vyombo vya usafiri Tanesco Mkoa wa Arusha kuimarisha utoaji huduma

📌 Ni katika muendelezo wa mkakati wa TANESCO wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi. 📌...