‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu

KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa kosa la walinzi wake kugombana na kutoleana lugha za matusi wakati wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo ulipigwa Machi 1,2026 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Adhabu hiyo imetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kwa mujibu wa kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi, Simba italazimika kulipa gharama za matengenezo ya mlango wa kuingilia chumba cha kufanyia mikutano ya wanahabari ambao walinzi wake walivunja ili kulazimisha  timu hiyo kuingia kwa kutumia chumba hicho  kwa ajili ya kuvalia kabla ya mchezo.

Pia mchezaji wa Simba David Kameta ametozwa faini y ash 1,000,000 kwa kosa la kuonekana akimwaga kimiminika kiwanjani dakika chache baada ya kuwasili uwanja wa Amaan kitendo kilichotafsiliwa kwa Imani za kishirikina.

Aidha Simba imetoza faini ya  jumla ya sh 10, 000,000 kwa makosa ya  kukataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia na kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi ambapo kila kosa imetozwa sh, 5, 000,000.

spot_img

Latest articles

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

More like this

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...