‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu

KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa kosa la walinzi wake kugombana na kutoleana lugha za matusi wakati wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo ulipigwa Machi 1,2026 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Adhabu hiyo imetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kwa mujibu wa kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi, Simba italazimika kulipa gharama za matengenezo ya mlango wa kuingilia chumba cha kufanyia mikutano ya wanahabari ambao walinzi wake walivunja ili kulazimisha  timu hiyo kuingia kwa kutumia chumba hicho  kwa ajili ya kuvalia kabla ya mchezo.

Pia mchezaji wa Simba David Kameta ametozwa faini y ash 1,000,000 kwa kosa la kuonekana akimwaga kimiminika kiwanjani dakika chache baada ya kuwasili uwanja wa Amaan kitendo kilichotafsiliwa kwa Imani za kishirikina.

Aidha Simba imetoza faini ya  jumla ya sh 10, 000,000 kwa makosa ya  kukataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia na kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi ambapo kila kosa imetozwa sh, 5, 000,000.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...