‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu

KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa kosa la walinzi wake kugombana na kutoleana lugha za matusi wakati wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo ulipigwa Machi 1,2026 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Adhabu hiyo imetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kwa mujibu wa kanuni ya 47:1 ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa klabu.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi, Simba italazimika kulipa gharama za matengenezo ya mlango wa kuingilia chumba cha kufanyia mikutano ya wanahabari ambao walinzi wake walivunja ili kulazimisha  timu hiyo kuingia kwa kutumia chumba hicho  kwa ajili ya kuvalia kabla ya mchezo.

Pia mchezaji wa Simba David Kameta ametozwa faini y ash 1,000,000 kwa kosa la kuonekana akimwaga kimiminika kiwanjani dakika chache baada ya kuwasili uwanja wa Amaan kitendo kilichotafsiliwa kwa Imani za kishirikina.

Aidha Simba imetoza faini ya  jumla ya sh 10, 000,000 kwa makosa ya  kukataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia na kuingia uwanjani kwa kutumia mlango usio rasmi ambapo kila kosa imetozwa sh, 5, 000,000.

spot_img

Latest articles

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex...

Mufti Zubeir asisitiza upendo, kupuuza wanaoneza chuki za kidini mtandaoni

Na Mwandishi Wetu MUFTI na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametoa...

More like this

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex...