Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu

MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa la kukataa bao halali la Simba wakati wa mchezo na Yanga ulichezwa Machi Mosi, 2026 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Ligi iliyotolewa leo baada ya kikao cha Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kilichokaa Machi 4, 2026 kupitia mwenendo wa matukio mbalimbali ya ligi, mwamuzi huyo ambaye alikuwa msaidizi namba moja katika mchezo huo alishindwa kutafsiri vyema sheria za miguu.

Taarifa ya wataalamu wa kutafsiri sheria za soka baada  kufanyia tathmini ya video ya tukio imebaini kuwa hakukuwa na kola lolote kabla ya kufungwa kwa bao hilo.

Naye mwamuzi msaidizi namba mbili wa mchezo huo, Hamdan Said kutoka Mtwara amefungiwa miezi mitatu kwa kosa la kusimamisha mchezo katika dakika ya 61 ya mchezo, akisimamisha shambulizi Yanga dhidi ya Simba kwa kuashiria kimakosa kuwa mchezaji Prince Dube alikuwa katika eneo la kuotea.

Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa Kanuni ya 42:1(1.8) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti wa waamuzi.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...