Na Mwandishi Wetu
MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa Jumanne ya Disemba 16, 2025 katika Kijiji cha Ruanda, Mbinga mkoani Ruvuma.
Mhagama ambaye amekuwa Mbunge wa Peramiho kuanzia mwaka 2005, amefariki dunia jana Alhamisi, Disemba 11, 2025 jijini Dodoma.
Ratiba ya mazishi yake iliyotolewa usiku wa Alhamisi na uongozi wa Bunge, inaonesha Ijumaa, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Itega, jijini Dodoma.
Jumamosi ya Disemba 13, 2025, mwili wa Jenista utapelekwa Kanisa Katoliki Kiwanja cha Ndege itakapofanyika ibada.
Viongozi mbalimbali watahudhuria kanisani hapo wakiwemo Spika wa Bunge, Mussa Zungu, Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba na Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi.
Baada ya shughuli ya hapo kanisani, mwili wa Jenista utasafirishwa kwenda Songea, Mkoa wa Ruvuma.


