Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania ‘Tembo Warriors’ imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAAF) baada ya leo kuichapa Uganda mabao 4-1 katika michuano hiyo inayoendelea nchini Burundi.

Akizungumzia matokeo hayo, Kocha wa Tembo Warriors Ivo Mapunda, amesema ushindi huo umetokana na marekebisho ya kiufundi waliyofanya baada ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Kenya.

Amesema ilikuwa ni mechi ngumu lakini walipambana kwa sababu ilikuwa ni lazima washinde ili kuendelea na hatua nyingine ya mashindano.

” Leo ilikuwa ni lazima tushinde, nawashukuru wachezaji kwa kufuata maelekezo vizuri, tunachoangalia kwa sasa ni mchezo wetu wa kesho na Burundi ambao ni lazima tushinde ili tuingie fainali,” amesema Mapunda.

Mchezo wa kwanza timu hiyo ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-0 na Kenya ambayo ndiyo inayoongoza kundi B ikiwa na pointi sita, Tanzania ya pili na alama tatu.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...