Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania ‘Tembo Warriors’ imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAAF) baada ya leo kuichapa Uganda mabao 4-1 katika michuano hiyo inayoendelea nchini Burundi.

Akizungumzia matokeo hayo, Kocha wa Tembo Warriors Ivo Mapunda, amesema ushindi huo umetokana na marekebisho ya kiufundi waliyofanya baada ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Kenya.

Amesema ilikuwa ni mechi ngumu lakini walipambana kwa sababu ilikuwa ni lazima washinde ili kuendelea na hatua nyingine ya mashindano.

” Leo ilikuwa ni lazima tushinde, nawashukuru wachezaji kwa kufuata maelekezo vizuri, tunachoangalia kwa sasa ni mchezo wetu wa kesho na Burundi ambao ni lazima tushinde ili tuingie fainali,” amesema Mapunda.

Mchezo wa kwanza timu hiyo ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-0 na Kenya ambayo ndiyo inayoongoza kundi B ikiwa na pointi sita, Tanzania ya pili na alama tatu.

spot_img

Latest articles

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...

Mpina ashinda kesi, ruksa kugombea Urais

Na Mwandishi Wetu Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba...

Mahakama kuamua hatma ya Lissu Jumatatu

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Tundu Lissu,  amerejeshwa...

More like this

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...

Mpina ashinda kesi, ruksa kugombea Urais

Na Mwandishi Wetu Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba...