Kijana ahukumiwa jela miaka 30 kwa kubaka mzee wa miaka 80 kichakani

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani, imemhukumu Said Nawanje (20) mkazi wa Yombo Lukinga, wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mzee wa miaka 80.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Juni Mosi, 2025 huko Kijiji cha Yombo Lukinga, Kisarawe baada ya kumvizia bibi huyo akitoka shambani ambapo alimtishia kisu kisha kumsukuma kichakani na kumbaka.

Hukumu hiyo ya kesi namba 15006/2005 imesomwa Agosti 20, 2025 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, Simon Mosses baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri.

Hakimu Mosses alieleza kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130 (1), (2) (a) na 131 (1) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...