Kijana ahukumiwa jela miaka 30 kwa kubaka mzee wa miaka 80 kichakani

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani, imemhukumu Said Nawanje (20) mkazi wa Yombo Lukinga, wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mzee wa miaka 80.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Juni Mosi, 2025 huko Kijiji cha Yombo Lukinga, Kisarawe baada ya kumvizia bibi huyo akitoka shambani ambapo alimtishia kisu kisha kumsukuma kichakani na kumbaka.

Hukumu hiyo ya kesi namba 15006/2005 imesomwa Agosti 20, 2025 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, Simon Mosses baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri.

Hakimu Mosses alieleza kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130 (1), (2) (a) na 131 (1) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...