Polisi feki wakamatwa Pemba

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kujifanya askari Polisi wa kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Watuhumiwa hao ni Abdulkadir Uwiso (55) mfanyakazi wa kampuni ya ulinzi na mkazi wa Buza na Khalfani Molo (60) mfanyabiashara wa Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi Mkoa Kaskazini Pemba, watu hao walifika katika Kijiji cha Konde na kujitambulisha kuwa ni maafisa wa Polisi kutoka Makao Makuu ndogo ya Polisi Dar es Salaam, kitengo cha uchunguzi wa magari yaliyoibiwa.

Taarifa hiyo inasema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa katika Stendi ya Konde wakiwa tayari wamekamata gari moja ya abiria aina ya Coaster yenye namba za usajili Z510MY ambapo walimtaka dereva wa gari hiyo, Said Nassor Ali kituoni wakidai ni gari la wizi lililoibiwa Msumbiji.

Baada ya watuhumiwa kufanyiwa upekuzi walikutwa na redio call moja, funguo ya pingu na filimbi ya Jeshi la Polisi.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...