Rais Samia kuzindua ujenzi wa matanki 15 ya mafuta Bandari ya Dar es Salaam

Na Tatu Mohamed

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa matanki 15 ya kuhifadhia mafuta itakayofanyika Machi 3, 2026, katika Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza Machi 2, 2026, Waziri wa Uchukuzi, Makame Mbarawa, amesema hafla hiyo ni sehemu ya mpango mpana wa Serikali wa kupanua na kuboresha bandari hiyo ili kuimarisha nafasi yake kama lango kuu la biashara nchini na katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Prof. Mbarawa ameeleza kuwa ujenzi wa matanki hayo 15 utaongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa taifa katika kuhifadhi mafuta, kuboresha mnyororo wa usambazaji wa nishati, na kuchochea ukuaji wa biashara za ndani na za kimataifa.

Amesisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji katika eneo la ukanda.

“Mradi huu unaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha miradi ya kimkakati inayochochea maendeleo ya nchi,” amesema Prof. Mbarawa.

Maboresho hayo ni sehemu ya uwekezaji unaoendelea katika Bandari ya Dar es Salaam, yakilenga kuongeza ufanisi wa huduma, kuvutia wawekezaji zaidi, na kuimarisha ushindani wa bandari hiyo katika soko la kimataifa.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

MD Twange aeleza kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa mradi wa Hale

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa...

More like this

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...