CCM yaomba kuchangiwa bilioni 100 za kampeni

Na Mwandishi Wetu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinahitaji kupata sh 100 bilioni kwa ajili ya shughuli za kampeni kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na waandishi na wahariri wa habari leo Agosti 11,2025, jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa CCM ambaye pia ni mgombea mwenza wa Urais, Dk. Emmanuel Nchimbi ameviomba vyama shindani vya siasa kuichangia CCM sambamba na wanachama na wadau wengine.

Amesema harambee ya kuchangia kampeni za chama hicho inatarajia kuzinduliwa rasmi kesho katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ikiwa ni kwa ajili ya maandalizi ya kampeni katika kugharamia magari, mabango, mafuta, fulana na kanga.

Dk. Nchimbi amesema uamuzi wa kuandaa harambee hiyo umetokana na hamasa kubwa iliyojitokeza kwa wanachama kutaka kuchangia kampeni.

“Kwa wakati ule kulitokea hamasa kubwa kwa wanachama wa CCM kutamani kuchangia michango ya kampeni. Kutokana na hamasa hiyo, sisi kama Kamati Kuu tumeamua sasa kuwashirikisha wanachama wetu katika uchangiaji kesho saa 11 jioni katika ukumbi wa Mlimani City,”


Vilevile, Dk. Nchimbi amefungua milango kwa vyama vingine kuchangia katika kampeni hiyo ambapo amesema kuwa;

“Kuhusu vyama vingine, tutafarijika sana vikichangia, kwa sababu haihitaji ushahidi wa kipolisi kujua CCM inatumikia watanzania na vyama vingine vyote,”

Akizungumzia kuhusu udhibiti wa fedha haramu, amesema “Jitihada yetu kubwa sisi kama CCM ni kujiepusha kuwa Serikali, kwa hiyo sisi siyo taasisi ya uchunguzi wa fedha haramu. Wenye kazi yao wataendelea kutafuta fedha hizo, sisi tutaendelea kufanya kazi ya siasa, kwa maana kitu kinachoharibu nchi ni chama cha siasa kuendelea kufanya kazi za dola,” ameeleza.

spot_img

Latest articles

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...

MAB yateta na wadhibiti Mutukula OSBP

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB), Eric Shitindi...

More like this

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...