Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu

WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Al-MahaTravel and Tours ambapo nafasi 1,150 za kazi ya udereva wa mabasi ya mwendo kasi zinapatikana nchini Qatar.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Al-Maha Travel, Abdallah Mohamed, alisema mchakato wa usaili utaendeshwa kwa uwazi na hautamhusisha mwombaji kugharamia fedha yoyote, huku akiwahimiza madereva wenye vigezo kujitokeza kuomba nafasi hizo kwa wakati.

Alisema waombaji wanapaswa kuwa na leseni halali ya udereva Daraja C au E, umri kati ya miaka 25 hadi 50, hati halali ya kusafiria pamoja na uwezo wa kuwasiliana kwa lugha za Kiingereza au Kiarabu.

“Aidha, waombaji wote watatakiwa kuthibitisha afya zao kabla ya kuajiriwa. Watakaofanikiwa kuchaguliwa watalipwa mshahara wa Dola za Marekani 700 kwa mwezi pamoja na marupurupu mengine ikiwemo bima ya afya, chakula na malazi bila gharama,” alisema.

Vilevile, aliongeza kuwa gharama za tiketi ya ndege zitagharamiwa na mwajiri.

Alifafanua kuwa mwisho wa kupokea maombi ni Februari 04, 2026 na usaili utafanyika kuanzia Februari 6 hadi 8, 2026, ambapo madereva 900 wanahitajika kutoka Tanzania Bara na 250 kutoka Zanzibar.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...