CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu 

BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini kwa kuweka mifumo ya kifedha itakayowawezesha wabunifu kubadili vipaji vyao na kuwa biashara endelevu zenye mchango wa moja kwa moja katika uchumi wa Taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa Jukwaa la Mitindo Tanzania, Meneja wa Huduma kwa Wateja Wadogo na wa Kati kutoka Benki ya CRDB, Japhary Hassanal, amesema kuunganisha ubunifu na mifumo ya biashara ni hatua muhimu katika kuimarisha mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya nchi.

“Lengo letu ni kuona ubunifu uliopo unageuzwa kuwa biashara zenye tija, ajira na mchango halisi katika uchumi wa Taifa,” amesema Japhary.

Ameeleza kuwa CRDB inatambua nafasi ya sekta ya mitindo katika kukuza biashara ndogo na za kati, ajira kwa vijana na wanawake pamoja na kupanua wigo wa uchumi wa ubunifu nchini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wabunifu Tanzania (FAT), Mustafa Hassanal, amesema tasnia ya mitindo ina uwezo mkubwa wa kuchochea uchumi kupitia viwanda, biashara na diplomasia ya kiuchumi endapo itawekewa mifumo imara na sera rafiki.

“Mitindo leo si suala la urembo pekee, bali ni sekta ya kimkakati inayogusa ajira, biashara na utambulisho wa Taifa,” amesema Hassanal.

Ameongeza kuwa kwa muda mrefu mitindo barani Afrika imekuwa ikionekana kama kipaji kisicho na mifumo madhubuti ya kifedha na kibiashara, hali iliyodhoofisha ukuaji wa sekta hiyo licha ya kuwepo kwa vipaji vingi.

Hassanal amesema Jukwaa la Mitindo Tanzania limeanzishwa ili kuwakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto na kuweka mikakati ya vitendo ya kuigeuza mitindo kutoka kipaji binafsi na kuwa sekta rasmi ya uchumi wa Taifa.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...