CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu 

BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini kwa kuweka mifumo ya kifedha itakayowawezesha wabunifu kubadili vipaji vyao na kuwa biashara endelevu zenye mchango wa moja kwa moja katika uchumi wa Taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa Jukwaa la Mitindo Tanzania, Meneja wa Huduma kwa Wateja Wadogo na wa Kati kutoka Benki ya CRDB, Japhary Hassanal, amesema kuunganisha ubunifu na mifumo ya biashara ni hatua muhimu katika kuimarisha mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya nchi.

“Lengo letu ni kuona ubunifu uliopo unageuzwa kuwa biashara zenye tija, ajira na mchango halisi katika uchumi wa Taifa,” amesema Japhary.

Ameeleza kuwa CRDB inatambua nafasi ya sekta ya mitindo katika kukuza biashara ndogo na za kati, ajira kwa vijana na wanawake pamoja na kupanua wigo wa uchumi wa ubunifu nchini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wabunifu Tanzania (FAT), Mustafa Hassanal, amesema tasnia ya mitindo ina uwezo mkubwa wa kuchochea uchumi kupitia viwanda, biashara na diplomasia ya kiuchumi endapo itawekewa mifumo imara na sera rafiki.

“Mitindo leo si suala la urembo pekee, bali ni sekta ya kimkakati inayogusa ajira, biashara na utambulisho wa Taifa,” amesema Hassanal.

Ameongeza kuwa kwa muda mrefu mitindo barani Afrika imekuwa ikionekana kama kipaji kisicho na mifumo madhubuti ya kifedha na kibiashara, hali iliyodhoofisha ukuaji wa sekta hiyo licha ya kuwepo kwa vipaji vingi.

Hassanal amesema Jukwaa la Mitindo Tanzania limeanzishwa ili kuwakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto na kuweka mikakati ya vitendo ya kuigeuza mitindo kutoka kipaji binafsi na kuwa sekta rasmi ya uchumi wa Taifa.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...