VETA Kihonda yabuni mashine ya kusaga chumvi, kuinua thamani ya zao hilo

Na Tatu Mohamed, Dodoma

CHUO cha VETA Kihonda kimebuni mashine mpya ya kusaga chumvi ya mawe, hatua inayolenga kuongeza thamani ya zao hilo na kurahisisha matumizi yake katika sekta mbalimbali.

Akizungumza kwenye Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, Mkufunzi Mwandamizi wa chuo hicho, Fredrick Uliki, amesema mashine hiyo imeundwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia wakulima wadogo wa chumvi hususani wa Bagamoyo na Lindi ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kusaga chumvi.

“Chumvi inapokuwa unga, matumizi yake yanapanuka zaidi. Kwa mfano, kwenye nyama ya kuchoma au chakula cha mifugo, ni lazima utumie chumvi ya unga. Pia, chumvi ikisagwa ni rahisi kuongeza madini joto na virutubishi vingine,” amesema Uliki.

Amefafanua kuwa, Mashine hiyo ina uwezo wa kusaga kilo 100 hadi 150 kwa saa, na imetengenezwa kwa malighafi imara zisizoshika kutu, jambo linaloifanya idumu kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Uliki, teknolojia hiyo inalenga kusaidia wakulima kuongeza thamani ya chumvi yao, kuisafirisha kwa urahisi zaidi na kupata soko pana.

spot_img

Latest articles

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

MD TWANGE ATOA RAI KWA MAMENEJA TANESCO KUONGEZA KASI YA KUPAMBANA NA WIZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME

📌Afungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, Dodoma 📌Asisitiza umuhimu wa...

Yanga yakomaa kileleni, Simba yavizia ikitafuna  miwa Morogoro

Na Mwandishi Wetu WANANCHI Yanga wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu...

WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTUMIA NISHATI SAFI EXPO KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati inaendelea kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia...

More like this

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

MD TWANGE ATOA RAI KWA MAMENEJA TANESCO KUONGEZA KASI YA KUPAMBANA NA WIZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME

📌Afungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, Dodoma 📌Asisitiza umuhimu wa...

Yanga yakomaa kileleni, Simba yavizia ikitafuna  miwa Morogoro

Na Mwandishi Wetu WANANCHI Yanga wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu...