VETA Kihonda yabuni mashine ya kusaga chumvi, kuinua thamani ya zao hilo

Na Tatu Mohamed, Dodoma

CHUO cha VETA Kihonda kimebuni mashine mpya ya kusaga chumvi ya mawe, hatua inayolenga kuongeza thamani ya zao hilo na kurahisisha matumizi yake katika sekta mbalimbali.

Akizungumza kwenye Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, Mkufunzi Mwandamizi wa chuo hicho, Fredrick Uliki, amesema mashine hiyo imeundwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia wakulima wadogo wa chumvi hususani wa Bagamoyo na Lindi ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kusaga chumvi.

“Chumvi inapokuwa unga, matumizi yake yanapanuka zaidi. Kwa mfano, kwenye nyama ya kuchoma au chakula cha mifugo, ni lazima utumie chumvi ya unga. Pia, chumvi ikisagwa ni rahisi kuongeza madini joto na virutubishi vingine,” amesema Uliki.

Amefafanua kuwa, Mashine hiyo ina uwezo wa kusaga kilo 100 hadi 150 kwa saa, na imetengenezwa kwa malighafi imara zisizoshika kutu, jambo linaloifanya idumu kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Uliki, teknolojia hiyo inalenga kusaidia wakulima kuongeza thamani ya chumvi yao, kuisafirisha kwa urahisi zaidi na kupata soko pana.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...